WENYEVITI WA MAJIMBO CHADEMA MBEYA WAUNGANA KUMUUNGA MKONO TUNDU LISSU WAMKATAA MBOWE, WATOA TAMKO
Viongozi mbalimbali wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutoka majimbo manne na wilaya moja mkoani humo wameeleza kuafikiana kuhakikisha Januari 21, 2025 wanamchagua Tundu Antipas Lissu kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Taifa. Akizungumza na waandishi wa habari Januari 09,2025 jijini Mbeya, kiongozi wa umoja huo wa wenyeviti na makatibu wa !majimbo ya mkoa wa Mbeya Peter Mwashiti ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Mbarali amesema mwenyekiti anayemaliza muda wake Freeman Mbowe amefanya kazi kubwa ya kukijenga Chama hicho lakini kwa sasa Tundu Lissu ndiye mwenye uwezo wa kuleta mabadiliko yanayotarajiwa na wanachama na wananchi kwa ujumla. "Tuko hapa kueleza msimamo wetu kuwa tunamuunga mkono Lissu kwasababu baada huu mchakato wa uchaguzi kuanza tulikuwa tunapokea maoni mengi sana kutoka kwa wanachama, mfano Kyela tulivyofika sio kwamba tulifika tu kwa viongozi hapana tulionana na wanachama na wazee tukasikia maoni yao na wanachama wamekata tamaa sana tunahitaji mtu wa kutuamsha. Nikama Musa alivyowaongoza wana wa Israel kutoka Misri kwenda Kanani Musa hakufika ila alimwachia Joshua akawafikisha nchi ya ahadi kwahiyo Chama na wanachama kwa sasa wanamtaka Tundu Lissu", amesema Mwashiti. Naye mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Mbeya vijijini Getruda Lengesela, amesema huu ni wakati wa kutishwa hivyo kutokana na kazi nzuri ya kukijenga CHADEMA chini ya mwenyekiti Mbowe ikiwemo kuwajengea uwezo wanawake lakini kwa sasa Chama hicho kinamhitaji Tundu Lissu ili kuendeleza uhai wa Chama hicho kufikia malengo ya kushika dola. Ande Kyamba ni mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Busokelo anasema Tundu Lissu ana kura za kutosha katika jimbo hilo na mkoa wa Mbeya kwa ujumla. "Kama tutapuuza maoni ya wanachama madhara ni makubwa, harakati zinaweza kupungua sana, sasa hivi watu wanajitambua tofauti na zamani Lissu na Mbowe wameshajipambanua na wanachama wameshawapima na wanajua kwamba Tundu Lissu anaweza hata ukiweka mkutano hapa leo ukawauliza wananchi nani aje Mbowe na Lissu watamtaka Lissu, tumetoka kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa chama Taifa hakijafanya chochote badala yake sisi huku na wanachama na wananchi tumejichangisha na kufanikisha Serikali za mitaa kwahiyo tusipoheshimu mawazo ya wananchi chama kitakosa uungwaji mkono hata kwa wadau wetu Mbowe miaka ishirini aloyofanya inatosha", amesema Ande Kyamba mwenyekiti wa CHADEMA jimbo la Busokelo. Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa CHADEMA Taifa kutoka mkoani Mbeya wanasema adui yao mkubwa ni Chama Cha Mapinduzi hivyo wanaamini Tundu Lissu na mgombea wake wa u-makamu John Heche ndio wenye uwezo wa kupambana na CCM kwa sasa. Wamesema tarehe 21 Januari 2025 baada ya uchaguzi watahakikisha wanarudi na jina la wakili Tundu Antipas Lissu Mugwai kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na John Heche kuwa makamu mwenyekiti wa CHADEMA Taifa (bara) ambapo majimbo yaliyojitokeza hadharani kutoa msimamo huo ni Mbarali, Mbeya vijijini, Lupa, Busokelo na Wilaya ya Rungwe na uchaguzi wa CHADEMA Taifa unatarajiwa kufanyika Januari 21, 2025.

🔴#BREAKING: MATOKEO RASMI UCHAGUZI CHADEMA YATANGAZWA - LISSU AIBUKA KIDEDEA - AMPIGA MBOWE kwa 3%..

PART 2: MBOWE 'AWAKA' LISSU HANA SHUKRANI, UCHAGUZI UWE LIVE, MKINIKATAA NARUDI NYUMBANI

KAKA YAKE TUNDU LISSU AONGEA, AKERWA NA KAULI ZA LISSU NA MBOWE "SISI TUPO TOFAUTI"

HECHE AONGEZEWE ULINZI, KAULI YAKE YATIMIA?, "CCM HAMUWEZI KUSHINDANA NA CHADEMA, MTAPASUKA KIFUA"

"MSIPOTULETEA LISSU MBAKI HUKOHUKO" WANACHAMA CHADEMA MBEYA WATANGAZA VITA NA WAJUMBE KUTOKA MBEYA.

🔴#LIVE: CHADEMA WAITIKISA MPANDA MJINI WASEPA NA KIJIJI, HECHE,MNYIKA, WAUWASHA MOTO

" CHADEMA MKOA WA SONGWE WAMKATAA RASMI MBOWE '' TUNAMTAKA LISSU''

🔴#Live: KIMEUMANA! UCHAGUZI MKUU CHADEMA - TIMU MBOWE na LISSU HAPAKALIKI- POLISI WAPO KULINDA AMANI

LUSAKO ASIMAMA NA TUNDU LISSU KINYANG'ANYIRO CHA UCHAGUZI CHADEMA/ AMSHUKIA VIKALI MBOWE

VIONGOZI WA MAJIMBO YA MKOA WA MBEYA WATOA TAMKO KUMUUNGA MKONO LISSU

Mapya yaibuka kuelekea Uchaguzi Mkuu ndani ya CHADEMA

HECHE: MKE WA TUNDU LISSU NA DADA YAKE POLE POLE WAMEUWASHA MOTO BUNGE LA ULAYA

"Kumrudisha Mbowe Kwenye Uenyekiti Tunajitakia Matatizo"Wafuasi wa CHADEMA Mbeya

NONDO ZA MNYIKA TABORA MJINI ZINAFIKILISHA NI BALAA TUPU "KATAMBI HANA UBAVU WA KUTAMKA MANENO YALE"

CHADEMA MKOA WA MARA WATOA TAMKO ZITO LA KUMUUNGA MKONO LISSU "MBOWE SIYO MWANZILISHI WA HIKI CHAMA"

"SERA ZA LISSU ZITAAMSHA CHAMA" KATIBU WA CHADEMA JIMBO LA LUPA AFUNGUKA MAZITO

🅻🅸🆅🅴 CHADEMA DODOMA WANATANGAZA MAAMUZI YA KUMUUNGA MKONO LISSU, WAMKATAA MBOWE

Inside Little Asmara in Uganda, Eritrean City Away From Eritrea 🇪🇷 (Eritrean Community)

BALAA! MZEE WA CHADEMA MBEYA AUWASHA MOTO MBELE YA LISSU NA HECHE, AWATWANGA CCM BILA HURUMA

