Sikio la Kufa: Daktari Feki Aliyenaswa Muhimbili, Adakwa Tena Amana, Cheki Ilivyokuwa
Mkazi wa jiji la Dar es Salaam, Abdallah Juma aliyewahi kukamatwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) akidaiwa kujifanya daktari amenaswa tena katika Hospitali ya Rufaa ya Amana kwa kufanya kazi katika hospitali hiyo wakati sifa za udaktari hana. Juma amenaswa akijifanya daktari, baada ya kuwekewa mtego na uongozi wa hospitali hiyo. Kukamatwa kwa Juma kunakuja ikiwa ni miezi mitatu tu imepita tokea Juni 19 mwaka huu alipo kamatwa katika hospitali ya Muhimbili kwa kujifanya daktari. Katika hospitali ya Muhimbili kijana huyo alijifanya kutoa huduma katika maabara kuu huku uongozi ukiwa hauna taarifa ya kuwepo kwa huduma aliyokuwa akiitoa kitu ambacho kilisababisha kushtukiwa na kukamatwa. Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Amana, Zainab Hoti akizungumza waandishi habari juu wananchi kuacha njia ya mkato katika kupata huduma katika hospitali ya Amana. Baada ya kukamatwa Uongozi wa hospitali hiyo ulifanya uchunguzi na kubaini kuwa kijana huyo hakuwa daktari bali daktari feki kama alivyokuwa akijitambulisha na kwamba amekamatwa mara baada ya kuwekewa mtego na askari wa hospitali hiyo. Daktari wa Kitengo cha Watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (WAVIU), Shani Mwaruka alikiri kukamatwa kwa kwa mtuhumiwa huyo. Amesema, Juma alinaswa baada ya uongozi kupata malalamiko kutoka kwa watu waliokuwa wakihitaji huduma katika hospitalini hiyo. Amesema tayari hospitali hiyo iliweka mtego imara wa maofisa wake, ambapo Juma aliingia bila hofu yeyote na kukutana na watu ambao alitaka wampe fedha ili awahudumie ndipo aliponaswa. Baadhi ya watu waliodaiwa kuombwa fedha na daktari huyo feki, wamesema aliahidi kuwatafutia kazi mbalimbali katika hospitali hiyo. Daktari wa Kitengo cha Watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (WAVIU) wa Hospitali ya Amana, Shani Mwaruka akizungumza na waandishi wa habari juu ya kumnasa Daktari ‘feki’ katika hospitali hiyo leo jijini Dar es Salaam. Nae mwananchi aliyekwenda kupata huduma hospitali ya Amana Cecilia amesema Agosti 9 mwaka huu, kijana huyo aliwaeleza kuwa kuna kazi katika hospitali ya Amana na yeye kama daktari bingwa anayefanya kazi hapo anaweza kuwasaidia. “Alituambia kuwa fomu zinatolewa katika hospitali ya muhimbili sh. 150,000 lakini kwakuwa wao ni madakatari atatufanyia kwa sh. 100,000 tu. Tulichanga fedha hiyo na ilifikia 800,000 tukampatia,” alieza Cecilia. Ameongeza,Juni 19 mwaka huu aliwaita katika hospitali ya Amana ili kufanyiwa usahili lakini hakutokea na simu akawa hapokei. “Tuliamua kuuliza kwa madakatari kama wanamfahamu lakini hakuna aliyemfahamu ndipo tulipobaini kwamba tumetapeliwa na kuamua kufanya mtego kwa kushirikiana na uongozi uliofanikisha kumnasa leo ,” alieleza.

DAKTARI FEKI ADAKWA MUHIMBILI "MIMI NI OSTADHI MBAGALA NATAPELI TU"

Daktari feki mikononi mwa Polisi Mbeya

MNH - AFYA PODCAST: Fahamu kuhusu Kiharusi (Stroke) na Prof. Mohamed Janabi

Umunsi Inkotanyi zihashya EX-FAR kuri burende ya Kagugu - Ubuhamya bwa Maj Gen (Rtd) Sam Kaka

#TAZAMA| DAKTARI FEKI ADAKWA MUHIMBILI "MIMI NI OSTADHI MBAGALA"

DAKTARI FEKI WA OPARESHENI ZA MABUSHA AKAMATWA NJOMBE

Daktari feki anaswa Muhimbili

#TBC1: KISHINDO CHA AWAMU YA SITA | HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA

RAIS DKT MAGUFULI AZUNGUMZA NA WAFUNGWA NA MAHABUSU KATIKA GEREZA LA BUTIMBA JIJINI MWANZA

Teens unable to walk, mothers with rash-covered babies: How Kush is ruining lives

Polisi feki akamatwa jijini Dar es Salaam

MBUNGE WA KATAVI AVUNA PESA BUNGENI BAADA YA KUGONGA NONDO ZITO JUU YA UVUNJIFU WA MAADILI.

DKT.FEKI ALIYEKAMATWA MUHIMBILI AKAMATWA TENA HOSPITALI YA AMANA,AKITAKA KUTAPELI WAGONJWA

WAUZA MAGARI MAARUFU WASHANGAA SERIKALI KUNUNUA COSTA MOJA kwa MILIONI 300!..

DAKTARI FEKI AKAMATWA AKITIBU WAGONJWA NYUMBANI KWAKE "AMEHUDUMIA WATU 119 DAWA ZIME-EXPIRE"

MUONEKANO MPYA WA HOSPITALI YA MUHIMBILI, PROF JANABI AFAFANUA HUDUMA YA KUEGESHA MAGARI

AHMED GHAILAN: MTANZANIA ALIYETIKISA DUNIA KWA UGAIDI, AKIMSAIDIA OSAMA, AKAFUNGWA MAISHA GUANTANAMO

🔴LIVE: MWENYEKITI TAIFA ACT WAZALENDO OTHMAN MASOUD ANAFUNGUKA MUDA HUU

MGANGA MKUU WA HOSPITALI YA AMANA AFUNGUKA KUHUSU KUKAMATWA KWA DAKTARI FEKI.

