KAMATI YA SIASA MKOA WA LINDI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.
Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Lindi, leo, Mei 08,2025 imetembelea na kukagua miradi ya maenendeleo kuona namna ilani ya Chama hicho inavyotekelezwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi. Kamati hiyo ikiongozwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Cde. Daudi Msungu imeridhishwa na hatua za utekelezaji wa miradi ya maendeo waliyoitembelea ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na mingine imekamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi. Miradi iliyotembelewa ni upanuzi wa mradi wa Maji Kilangala,ujenzi wa Zahanati Kilangala,ujenzi wa shule ya Msingi ya ghorofa Likong'o, ujenzi shule mpya ya Sekondari Hamida Alkassim iliyopo kata ya Rasbura pamoja na ukarabati wa shule mpya ya mkondo mmoja shule ya Msingi Stadium. Msungu amesema miradi hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya awamu ya sita ya kupeleka maendeleo kwa Wananchi kupitia miradi inayogusa maisha yao moja kwa moja huku akipongeza usimamizi mzuri unaofanywa na viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi na kusisitiza kuwa utekelezaji wa miradi unapaswa kuendana na thamani ya fedha inayotumika. Aidha, amewahamasisha Wananchi wa Manispaa ya Lindi kushiriki kikamilifu katika zoezi la uboreshaji wa taarifa zao kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili litakalofanyika Mei 16 hadi 22, 2025, ambapo amesema hatua hiyo ni muhimu kwa ajili ya ushiriki wao katika mchakato wa kidemokrasia. Nao Wananchi walioshiriki mapokezi ya ziara hiyo Kwa kata mbalimbali ambazo kamati hiyo imepita kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameonesha furaha na kupongeza juhudi za serikali na chama katika kuhakikisha huduma muhimu zinawafikia, huku wakiahidi kuendelea kushirikiana na serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Niederlande – Japan Highlights | Gruppe F, FIFA WM 2026 | sportstudio

CHALAMILA ALIVYOAGIZA MWENYEKITI AKAMATWE na POLISI BAADA ya KUDAIWA KUTAPELI WATU VIWANJA....

HOSPITALI YA SOKOINE YAHAMIA MITWERO

Ruto heart attack as Sifuna and his troop holds Mega Rally in Thika with 'Sisi Ndio Sifuna!'

I left a life of luxury in America, only to come and live in isolation in Kenya | Tuko TV

Brasilien – Marokko Highlights | Gruppe C, FIFA WM 2026 | sportstudio

VIVUTIO NA FURSA ZA LI DI MANISPAA.

Why Aliens Would NEVER Invade Africa

UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%.

AMSHITAKI MMEWE KWA WAZIRI MKUU "ANAJINYEA TU" Wananchi Wavunjika Mbavu

How China Built an Impossible Bridge Above the Clouds

MIRADI 10 MIKUBWA YA UJENZI TANZANIA ITAKAYOKAMILIKA 2025

SERIKALI YATOA MAEKELEZO KWA WANANCHI WA WESTERN—LUHAFWE| HUDUMA ZENYE UTU KUWEZESHWA

I left Kenya to india for greener pastures, only to get myself in ashawo Jobs

DAWA YA RUTO!! Listen to Gachagua Powerful remarks today in Bungoma Church destroying Kasongo badly!

DC KALLI AINGILIA KATI KERO ZA MADEREVA WA MALORI LONGIDO

MOSHI DC HEALTH BOARD SATISFIED WITH SERVICE DELIVERY AND IMPLEMENTATION OF HEALTH PROJECTS

Urubanza rwa Agathon RWASA rugeze he?Kuki Amb.Cartas NJEBARIKANUYE yatumweko gihutihuti mu Burundi?

MTWARA YAFUNGUA FURSA MPYA KATIKA SEKTA YA CHUMVI-

