#live Kuwa na Yesu- Nyimbo za Kristo no 51 || Ben Chicco & Barrett Mapunda

Ungana na Ben Chicco @zee_masta, @barrettmapunda, pianist Jacob Mang'ombe @jacobmangombe na washiriki wa @mwengesdachurch kueleza furaha ya uzoefu wa wokovu mkuu aliotutendea Mungu wetu na furaha yako daima katika kumsifu Yeye kwa nyimbo... Nyimbo Za Kikristo No. 51: Kuwa Na Yesu 1. Yesu Mwokozi, kwa hakika, Hunipa furaha na amani; Mrithi wa wokovu wake, Natakaswa kwa damu yake. Habari hiyo wimbo wangu, Daima nitamsifu Yesu. Habari hiyo wimbo wangu, Daima nitamsifu Yesu. 2. Nijitoapo nina raha, Na kwa imani namwona Bwana; Aniletea malaika, Wananilinda, niokoke. 3. Hali na mali anaitwaa, Katika Yesu nabarikiwa; Nikimngoja kwa subira, Wema wake unanitosha. Wimbo huu uliimbwa katika #ibada maalum ya nyimbo, Jumamosi ya tarehe 26 Novemba 2023, katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Mwenge, #daressalaam. Tangu asubuhi hadi jioni kulikuwa na Ibada iliyojaa nyimbo na uimbaji. Ibada hiyo ilikusanya waimbaji wa zamani waliowahi kuimba katika Kwaya ya Mwenge @mwengeadventistchoir katika nyakati mbalimbali, tangu mwaka 1980 ilipoanzishwa. Kanisa la @mwengesdachurch lilianza kama Kundi lililotengwa kutoka Kanisa la @sdachurchmagomeni na kuanza kusali katika Shule ya Msingi Mwenge mwaka huo. Katika Ibada hiyo ya nyimbo, nyimbo mbalimbali za nyakati tofauti ziliimbwa na kuwa kivutio na mbaraka kwa wengi walioshuhudia. Ulikuwa ni wakati mwema pia kwa wengi kukutana baada ya kutengana kwa muda mrefu. Kwa namna iliyovutia wengi, waimbaji wawili mama Esther Wansinyo na mama Anna Nyaruhucha walipewa zawadi kutambuliwa kuwa ndio pekee waliodumu kuimba katika kwaya hiyo kwa MIAKA 43, tangu ilipoanzishwa bila kukoma! Ibada hiyo ya uimbaji ilihudumiwa vema sana na waimbaji mahiri kutoka kwaya ya @kingongosdachoir_tz, @angelmagoti, @barrettmapunda, @sondayadihluacapella, @acacia_singers_tz, @remnant_generationsingers, @ay_mwenge_sda_church_tz, @amazingharps_choir_tz na Women of Faith- Mwenge Karibu tena msimu mwingine wa uimbaji kama huu. @hopechanneltz @hope_recording_studio @hopemedia_ect #mwengesdachurch Ukiwa na swali, uhitaji wa maombi, ubatizo wasiliana na Mchungaji kwa namba +255 677 048 069 au +255 784 458 957. Kama una ushauri usisite kutuma kwa namba +255 713 215 930 au barua pepe [email protected]. Tunapenda kukujulisha kupitia channel hii, kuna vipindi mubashara mbalimbali kila siku jioni kama; Ongeza Ujuzi, Afya ni Mtaji, Kona ya Watoto, Lijue Kanisa na Ibada mbalimbali na maombi. Karibu ku-SUBSCRIBE ili uwe sehemu ya wengi wanaobarikiwa: https://bit.ly/SUBSCRIBE-Now, watumie na marafiki pia. Karibu pia kutembelea tovuti yetu: www.mwengesdachurch.or.tz Mungu akubariki.