WANUNUZI WA PARACHICHI WAONYWA KUTUMIA MIZANI ZISIZOHAKIKIWA ZINAZOWAIBIA WAKULIMA
Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe kwa kushirikiana na Ofisi ya Wakala wa Vipimo Mkoa wa Njombe imewatahadharisha wanunuzi wa matunda ya parachichi dhidi ya matumizi ya mizani isiyohakikiwa, ikieleza kuwa tabia hiyo inachangia kuwanyima wakulima haki yao na kusababisha hasara katika biashara ya mazao. Onyo hilo limetolewa baada ya kukamatwa kwa mzani uliokuwa ukitumiwa na mnunuzi wa parachichi ambaye alibainika kutumia kifaa chenye upungufu wa kilo 1.35 kwa kila kilo 100 zinazopimwa. Akizungumza Juni 10, 2026 Afisa Kilimo,Halmashauri ya Mji Njombe, Bw. Baraka Mlawa, amesema hatua hiyo ilichukuliwa kufuatia taarifa zilizotolewa na mkulima Markus Ngole ambaye alitilia shaka usahihi wa vipimo vya mzani huo. Amesema baada ya kupokea taarifa hizo, maafisa wa kilimo walishirikiana na Ofisi ya Wakala wa Vipimo Mkoa wa Njombe kufanya ukaguzi wa mzani huo, ambapo walibaini kuwa ulikuwa haukidhi viwango vinavyotakiwa na ulikuwa ukiwasababishia hasara wakulima. “Tunawapongeza wakulima wanaotoa taarifa mapema wanapobaini dosari katika shughuli za biashara. Ushirikiano huu umewezesha kubaini tatizo na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria,” alisema Mlawa. Aidha, aliwahimiza wakulima wengine kuendelea kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapokutana na changamoto zinazohusiana na upimaji au ununuzi wa mazao yao ili kulinda maslahi yao. Kwa upande wake, Afisa Vipimo Mwandamizi Mkoa wa Njombe, Bw. Shabani Kiku, alisema uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa mzani huo haukuwa umehakikiwa na Wakala wa Vipimo na haukuwa ukitoa matokeo sahihi wakati wa upimaji. Alieleza kuwa upungufu wa kilo 1.35 katika kila kilo 100 zinazopimwa unaweza kusababisha hasara kubwa kwa wakulima kwa kuwa hupokea malipo yasiyoendana na uzito halisi wa mazao yao. Kiku aliwataka wakulima kuhakikisha wanunuzi wote wa parachichi wanaotumia mizani yenye nembo na alama rasmi za uhakiki kutoka Wakala wa Vipimo. Pia alionya kuwa mnunuzi yeyote atakayebainika kutumia mizani isiyohakikiwa au inayokiuka viwango vya vipimo atachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria na kanuni za vipimo nchini. Halmashauri ya Mji Njombe itaendelea kulinda maslahi ya wakulima kwa kuhakikisha biashara ya mazao inafanyika kwa uwazi, haki na kuzingatia sheria za vipimo ili kuongeza imani na tija katika sekta ya kilimo hususan kilimo cha Parachich

Storchennest Live Webcam in Bad Salzungen, Thüringen

NJOMBE TC YAONGEZA JUHUDI KUHAMASISHA ULIPAJI KODI YA PANGO LA ARDHI

SAVED BY THE MAID - 2026 latest Nigerian movies - Ray Adeka - Gift Anizoba , Princess Orji

START YOUR TUESDAY WITH FAITH | TODAY GOD IS GIVING YOU UNEXPECTED OPPORTUNITIES | FATHER FREDDY ...

TAZAMA MAKALA MAALUM YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2026 NJOMBE TC

MATUKIO WAKATI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MJI NJOMBE.

KWA UCHUNGU, AFISA ARDHI NUSURA ATOKWE NA MACHOZI AKIZUNGUMZIA MIGOGORO YA ARDHI

KESI YA UHAINI YA LISSU YAIBUKA MAPYA, CHADEMA WADAI POLISI WAMEPANGA VURUGU MAHAKAMANI

HECHE AMCHANA SAIDI ISSA MOHAMED AMUITA MSALITI SIO MWENZETU | ANATUMIKA ALIFUNGUA KESI YA UONGO.

HII NDIYO RISALA YA UTII KWA MHE. RAIS ILIYOSOMWA WAKATI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU NJOMBE TC 2026

Scars from Russia: Former KDF pilot narrates his escape from Russia war, going for days without food

Shell and Chevron Abandoned This Coastline. Dangote Just Bought In.

The Richest Family in CAMEROON & The Secrets Behind Their Fortune...

#LIVE: WANANCHI (YANGA SC) WANAJAMBO LAO MUDA HUU JANGWANI

DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | 11.06.2026 | Asubuhi | Swahili Habari leo | Podcast

China Versus the US: Kishore Mahbubani on a Zero-Sum Rivalry | The Mishal Husain Show

LIPA PANGO LA ARDHI KWA WAKATI ILI KUEPUKA LIMBIKIZO LA ADA NA USUMBUFU USIO WA LAZIMA.

DC NJOMBE AKABIDHI MAGARI 2/ MKANDARASI KUANZA KAZI YA UJENZI WA BARABARA NJOMBE MJINI

Alikiba & Harmonize - Utanionea (Clip Officiel)

