Heri Kabisa & Yote Ninayo Niliyapokea - Tabernacle Chrétien de Lubumbashi

Heri Kabisa & Yote Ninayo Niliyapokea - Tabernacle Chrétien de Lubumbashi Timecodes 00:00 - Heri Kabisa - Nyimbo za Mungu 138 03:34 - Yote Ninayo Niliyapokea - Nyimbo za Mungu 87 HERI KABISA - Nyimbo za Mungu 138 1. Heri kabisa, Yesu ni wangu! Ni Muchungaji, na mimi ni wake; Nimezaliwa mara ya pili, Ninasafishwa kwa damu yake. Chorus [ Yesu ni wimbo wa roho yangu, Nitamusifu hata milele ] BIS 2. Kule mbinguni kuna furaha Ju-u ya mwenye kutubu makosa; Nilisikia Neno la Mungu, Nilijitoa kwa Bwana Yesu. 3. Ninashukuru Yesu Mwokozi, Na roho yangu inashangilia; Mimi si kitu mbele ya Mungu, Kwa neema yake ananipenda. 4. Ninastarehe sasa kwa Yesu, Nina salama kutoka kwa Mungu; Ninangojea Yesu afike Kunipeleka kwake mbinguni. YOTE NINAYO NILIYAPOKEA - Nyimbo za Mungu 87 1. Yote ninayo niliyapokea kwa wema wake unaoenea; Mimi si kitu, namutegemea ; nimeokolewa ka ne-ema. Chorus Niliyekuwa nimetoroka, kwa pendo lake nimeokoka! [ Yesu ni mwema na mwenye rehema. Nimeokolewa kwa ne-ema ! ] BIS 2. Nilitembea zamani kwa zambi katika njia ya kufa, lakini Yesu alinitafuta polini ; nimeokolewa kwa ne-ema. 3. Nimetakaswa na Yesu Mwokozi, si kwa matendo na si kwa machozi, Ila kwa damu nina ukombozi ; nimeokolewa kwa ne-ema. 4. Raha ya mbingu imeni-ingia, kwa shangwe kubwa namufurahia. Kwa kuwa Yesu ’nanirehemia ; nimeokolewa kwa ne-ema. Heri Kabisa & Yote Ninayo Niliyapokea - Tabernacle Chrétien de Lubumbashi Nyimbo za Mungu 138 & Nyimbo za Mungu 87 #Maranatha