Mkono wa msaada wa Ujerumani kwa wakimbizi

Ujerumani imeendelea kuwa mstari wa mbele kuwasaidia wakimbizi wanaokimbia vita nchini Ukraine. Hivi sasa mamlaka za mji mkuu, Berlin, zinatumia maeneo mawili ya Uwanja wa Ndege wa zamani wa Tegel kama kambi za wakimbizi. Una neno gani la faraja kwa watu wote wanaolazimika kuacha nyumba zao na kukimbia mizozo duniani?