RC MOROGORO AWASHUKIA WAKWEPA KODI IFAKARA
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amemuagiza Kamanda wa Jeshi la Polisi Wilaya Kilombero kuwatia mbaloni wafanyabiashara watatu kwa tuhuma za kuhujumi uchumi wa nchi. Loata ametoa agizo hilo Januari 7 mwaka huu ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Shule za Sekondari kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza wanaotarajiwa kuanza masomo januari hapo 11, 2021. Aidha, Kukamatwa kwa wafanyabiashara hao kumetokana na madai ya kuuza bidhaa mbali mbali bila kuwa na leseni kutoka kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) hivyo kuhujumu uchumi wa nchi licha ya Serikali inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutilia Mkazo katika suala nzima la ulipaji kodi. Mkuu huyo wa Mkoa amebinisha baadhi ya bidhaa ambazo wafanyabiashara hao wamekuwa wakiuza bila kulipa kodi kwa Mamlaka husika, kuwa ni pamoja na Saruji katika maduka ya kuuza vifaa vya ujenzi ambapo wamekuwa wakiuza bidhaa hiyo bila kutoa risiti kwa wanunuzi. Sambamba na hayo, Loata ametoa agizo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania - TRA kufanya utafiti juu ya mfanyabiashara Didas Kessy Paul juu ya mifuko ya saruji inayoingia na kutoka, kutokana na kuchanganya mifuko isiyo na vigezo katika sehemu moja huku ikisemekana kuuzwa kwa wananchi. ‘’TRA Naenda vijijini nikirudi hapa nipate proper record ya huyu mfanyabiashara anaingiza mifuko mingapi na anatoaje’’ amesema Sanare Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Ismail Mlawa, amekiri kuwepo kwa wafanyabiashara ambao hawalipi kodi kwa muda mrefu huku akimtaja mmoja wa wafanyabiashara hao Ndg. Robert Mbilinyi amekuwa mmoja wa wafanyabiashara wasumbufu katika ulipaji kodi ndani ya Wilaya hiyo hali iliyopelekea kutozwa faini ya zaidi Mil.10 miezi miwili iliyopita. Naye, Afisa Mapato Wilaya ya Kilombero Amani Timotheo ametaja majina ya wafanyabiashara ambao wamekuwa wakifanya biashara bila kulipa kodi kuwa ni James Mwaisungu ambaye anajihusisha na uuzaji wa vifaa vya pikipiki na Ndg. Robert Mbilinyi muuzaji wa saruji.

'WAZEE WA ILE PESA TUMA KWA NAMBA HII' WAFIKISHWA MAHAKAMANI "WAPO 15, WAKAZI WA MOROGORO"

RC Morogoro atolea ufafanuzi maagizo aliyoyatoa kuhusu bonde la Kilombero

Hii Ndio Barabara ya kuelekea Hospitali ya Saratani. IFAKARA

MIKAKATI YA MKOA WA MOROGORO YAWEKWA WAZI MBELE MBIO ZA MWENGE WA UHURU.

RC MALIMA AENDELEA KUTOA ELIMU, WANANCHI KUONDOKA PORI LA AKIBA KILOMBERO.

Mawasiliano ya Barabara ya Ifakara–Malinyi Yakatika, Watu Wavushwa kwa Mitumbwi

BREAKING: Iran vows response after Israel strikes Hezbollah targets

MWENGE WA UHURU MLIMBA, RC MALIMA ASHIRIKI

KITUO CHA AFYA NAMWAWALA CHATOA SULUHISHO LA VIFO VINAVYOZUILIKA KWA WAGONJWA

MKIMBIZA MWENGE WA UHURU ATAKA UTUZAJI WA MIUNDOMBINU YA MAJI

MWENGE WA UHURU KUPITIA JUMLA YA MIRADI 63 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 50.9 MKOANI MOROGORO.

HAONGA AMCHANA MAKAVU MSIGWA "UFUTE YAKE MANENO YALE KWENYE GARI" PASCAL HAONGA AWASHA MOTO IRINGA

WADAU WA BARABARA MOROGORO WAWEKA MIKAKATI YA MATENGENEZO YA BARABARA.

Ifakara Town , Tanzania

VIJANA MOROGORO WANUFAIKA NA MRADI WA GSREI

Ifahamu Ifakara Mjini

VIDEO: Mafuriko yaondoa uhai wa Mtu mmoja Ifakara

OQHAWEKAZI TEAM BLUE OBUKA | ISIBAYA SAMADODA | EMKHANDLWINI | OBUKA

RC Malima aweka mikakati kulinusuru Pori la akiba Kilombero.

