Peke Yako | AIC Milimani Nairobi KE - Mabalozi Choir

Ni nani mwingine wa kuabudiwa, kusifiwa, kusujudiwa, kuinuliwa na kutukuzwa, kama si Mungu wetu mkuu aliyee juu. Mwenye kuiumba ardhi na mbingu, mwenye kutupa pumzi, uhai na afya, mwenye kutupa matamanio ya mioyo yetu, kutuongoza na kutulinda ni nani mwingine? Je hivi leo una sababu ya kusema kwamba ni Mungu peke yake wa kuinuliwa na kuabudiwa? Mbona usiungane nasi katika wimbo huu wa sifa na kumwinulia mtawala wetu utukufu wote! "Wajue kwamba wewe peke yako ambaye jina lako ni Mwenyezi-Mungu, ndiwe Mungu Mkuu juu ya dunia yote." Zaburi 83:18 Shukrani: Kanisa: AIC Milimani Nairobi-KE Kwaya: Mabalozi Choir Mwalimu: Daudi T. Shigela Producer: LMJ Studio Lokesheni: USIU