MBOZI YAONGOZA UKUSANYAJI MAPATO,MOMBA YASHINDWA KUFIKIA LENGO
Songwe, 15 Mei 2025 – Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Daniel Chongolo, ameongoza na kufungua rasmi kikao cha tathmini ya utekelezaji wa utendajikazi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa (Halmashauri) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Nselewa – Mlowo, Wilaya ya Mbozi. Katika kikao hicho, Mhe. Chongolo alitoa pongezi kwa Halmashauri ya Mbozi, Mji wa Tunduma na Ileje kwa kuvuka lengo katika ukusanyaji wa mapato. Hata hivyo, alizitaka Halmashauri za Momba na Songwe kuongeza juhudi, akibainisha kuwa bado ziko chini ya lengo kwa kufikia asilimia 85.75 tu. “Kuna vyanzo vimekusanya chini ya malengo na vingine havijakusanya kabisa tangu kuanza kwa mwaka wa fedha. Nitoe rai kwa Halmashauri kuhakikisha kuwa kila chanzo cha mapato kinakusanywa kwa asilimia mia moja au zaidi ifikapo Juni 30, 2025 – mwisho wa mwaka wa fedha wa 2024/2025,” alisisitiza Mhe. Chongolo. Aidha, Mkuu wa Mkoa alieleza umuhimu wa kusimamia kwa ufanisi miradi ambayo tayari imepokea fedha, akisema kuwa “miradi inayoletwa fedha, matokeo ndio matarajio ya kila mmoja. Tukishindwa kuyafikia matokeo, maana yake tumeshindwa kutimiza dhamira ya anayeleta fedha, lakini pia tumeshindwa kutimiza matarajio ya wananchi.” Kikao hiki ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Mkoa wa Songwe katika kuhakikisha uwajibikaji na ufanisi katika ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri.

MBUNGE MUSUKUMA AKIELEZA MAGUMU ALIYOPITIA KATIKA SIASA NA BIASHARA | M&S PODCAST

KWENYE MAZISHI YA AYATOLLAH ALI KHAMENEI, MCHUNGU AFICHUA UKIWA NA DOLA 100 WEWE NI TAJIRI IRAN

How Traore is Magically Growing Real Apples in Desert?

MUAMALA WA LAKI TANO WAMPONZA MTENDAJI WA KIJIJI MBOZI

Maelfu ya JWTZ Wajazwa Miji mikuu kuelekea maandamano ya saba saba; Samia Aingiwa na uoga mkuu sana

WAKILI MADELEKA acharuka AJIPANGA KUKIBURUZA CHUO CHA ARDHI MAHAKAMANI "WEWE UTAKIFUNGA CHUO"

Cleaner Anatoly Pretends to Be an Old Man in the Gym

Top 10 Coolest Moments in Westerns | MGM

Most Cheap Street food in Afghanistan | Kabuli pulao, Roasted Chicken, Biryani recipe, Punjabi Curry

Kenya'sTransformation Continue!| The Rironi–Mau Summit Highway Is Coming to Life 🇰🇪

Pres Mahama inspects Kasoa-Budumburam-Winneba Big Push Multimillion Dollar Highway Project 2

“You’ll Never Be Like Us.” Until 500KG Happened 🔥

Jonction Rocade Sud-Est –Aéroport Mokali une circulation réussie après le passage du chef de l’état

NERVOUS 12-Year-Old Who Can Sing Without Opening Her Mouth Earns Mel B's GOLDEN BUZZER!

94 Year-Old Grandmother Living Alone at the Edge of the World Far From Civilization

MCHUNGAJI HANANJA AMJIBU MZEE WA UPAKO KUSEMA WAKRISTO WENGI HAWAJUI BIBLIA // INJILI HAIPO HIVO...

"Soon u won't be a president's Son.." Akena Obote wonders why a 27th in hierarchy control everything

YOU Won’t Believe This 😱 Homeless 8 Years of Hair & Beard Transformation

China’s Giant Cassava Flour Factory Exposed

