BUKU 5 YAMTOA KIMAISHA KWA BIASHARA YA JUICE

NATALIE ni kati ya vijana wachache wenye nia ya uthubutu. Uthubutu wake ulianza miaka minne iliyopita, alipokuwa anasoma chuo IFM. Yeye na dada yake wakaanza kuuza juisi ya Matunda kwa kutembeza mitaani Sinza, wengi wakawa wanamshangaa, wengine wakawa wanamwambia, "wewe ulivyomzuri hivi unafanya biashara ya kutembeza juisi barabarani?" ila kwake ndo ilikuwa chachu ya kuendelea kupigana. . . Kwa uthubutu huo umemuwezesha kufungua sehemu yake mwenyewe inaitwa ZANANA JUICE BOX zaidi hajawa mbinafsi anapiga mishe hii na vijana wenzie, hii yote kuhakikisha kwa #NguvuMoja vijana wengine wanapata fursa kujifunza na kujitengenezea mkwanja ili maisha yaendelee.