REA YATOA MWONGOZO UWEZESHAJI UJENZI VITUO VIDOGO VYA MAFUTA VIJIJINI.
Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imedhamiria kuanzisha mpango wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (Dizeli na Petroli) maeneo ya vijijini ili kuondosha njia zisizo salama za uhifadhi wa mafuta hayo. Hayo yamesemwa na Mhandisi Miradi kutoka REA, Kelvin Tarimo wakati akitoa semina kwa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Ruvuma, Oktoba 5 mwaka huu kwa mwaliko wa Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga. Akizungumza na Wajumbe wa Baraza hilo, Mhandisi Tarimo alieleza mambo mbalimbali ikiwemo mwongozo wa ujenzi wa vituo hivyo kwa wale watakaokidhi vigezo na kupata mkopo wa kuvijenga. Alisema kuwa pamoja na mambo mengine, Mwongozo huo unaainisha bayana vigezo kwa mwombaji wa mkopo ambavyo vimegawanyika katika makundi mawili; kiufundi na kifedha. Mhandisi Tarimo alivitaja baadhi ya vigezo vya kiufundi kwa mwombaji kuwa ni pamoja na mtu binafsi au kikundi cha wajasiriamali kijijini kilichosajiliwa na Mamlaka husika au Serikali ya kijiji kuwa na kibali cha ujenzi kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA). Kigezo kingine ni mwombaji kuwasilisha kwa REA barua ya maombi ya mkopo wa ujenzi wa kituo au vituo vipya tu na siyo vinavyohitaji ukarabati au vilivyoanza kujengwa. Aidha, mwombaji atatakiwa kuwa na barua ya uthibitisho kutoka Halmashauri ya kijiji na Wilaya inayomruhusu kuendesha biashara ya kituo cha mafuta katika eneo aliloomba pamoja na kuwa na namba ya mlipa kodi (TIN Namba) kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania. Pia, alieleza kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na uthibitisho wa umiliki wa ardhi (Hati Miliki ya ardhi au Hati za kimila au uthibitisho wa umiliki wa ardhi) kutoka kwa Halmashauri ya Kijiji au Wilaya. Kingine ni kibali cha ujenzi kutoka Mamlaka husika pamoja na kujaza fomu ya kuonesha namna anavyokusudia kufanya biashara ya mafuta. Akieleza zaidi, Mhandisi Tarimo alisema fedha hizo za Mradi zitakazotolewa kama mkopo, ni sehemu ya juhudi za Serikali zinazolenga kuzuia kuhifadhi mafuta ndani ya nyumba kwa kutumia mapipa na chupa za plastiki katika kuuza mafuta ya petroli na dizeli kwa watumiaji wadogo kama vile waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda katika maeneo ya vijijini. “Hii ni kutokana na kukua na kuongezeka kwa matumizi ya bidhaa hizi katika shughuli za maendeleo maeneo ya vijijini,” alisema. Kiasi cha mkopo ni shilingi milioni 75 na riba yake ni asilimia tano ilhali marejesho yake ni hadi kipindi cha miaka saba. Mhandisi Tarimo ametoa hamasa kwa wananchi wote wenye nia kutembelea tovuti ya Wakala wa Nishati Vijijini ambayo ni www.rea.go.tz ili kusoma Mwongozo kamili wa utoaji na usimamizi wa mkopo wa uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vidogo vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini.

REA kuongeza mikopo nafuu ya ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini

WAZIRI SILAA ALIVYOKATAA RUSHWA YA MIL.300/=, KUTOKA KWA MATAJIRI WA KITUO CHA MAFUTA

EWURA YALEGEZA MASHARTI UJENZI WA VITUO VYA MAFUTA MAENEO YA VIJINI/ MENEJA WALTER CHRISTOPHER ANENA

KUMECHEMKA🔥 Angry Murkomen sends a FRESH WARNING to Gachagua on Goons in Protests & Maandamano 2027

SERIKALI YATENGA BIL.12 KUWEZESHA UJENZI WA VITUO VYA MAFUTA VIJIJINI

ZAIDI YA MAGARI 1000 YAMEWEKWA MFUMO WA GESI ASILIA DIT

🔴#live UZINDUZI SHELI YA MABENA BOMBAMBILI,MAMIA WAPEWA MAFUTA BURE WAFUNGUKA,MGENI RASMI AFUNGUKA

TAZAMA KITUO cha MAFUTA KIKUBWA -HOTELI -SUPER MARKET ya KISASA ya KANISA la PASTOR EZEKIEL NEW LIFE

BREAKING NEWS: Listen to What Gachagua said after Ndindi Nyoro ADDRESS TO THE NATION

ACHEZEA MFUMO WA PETROL STATION NA KUIBA MAMILION YA PESA

Standard Media responds to President Ruto's blackmail claims

Watch What Gachagua Said After the Gen Z Demos!

Ujenzi Wa Kituo Cha Mafuta - Vitu Vya kuzingatia Kupata Ubora na Muonekano Maridadi

Worst Plane Landing Fails Caught on Camera

Total Tanzania: Mshuhudie Mtanzania wa Kwanza Kumiliki Kituo cha Mafuta cha Total kupitia DODO.

How Traore is Magically Growing Real Apples in Desert?

Ujenzi Wa Kituo Cha Mafuta - Zingatia Ukubwa wa Kiwanja (Site Plan)

Kenya Literature Bureau Strategic Plan 2025-2030 Launch

KITUO CHA MAFUTA KWA MILIONI 50 INAWEZEKANA EWURA YAWEKA WAZI MBINU ZA UWEKEZAJI KWA WATANZANIA.

