JOSEPH MAINA NA CHOMBO KILICHOUMBIKA

JOSEPH MAINA KATIKA CHOMBO KILICHOUMBIKA Wahenga walisema ya kale ni dhahabu, ndivyo inavyojidhiridha katika sauti za gharama ambapo leo tunasikiliza Wimbo wa Chombo Kimeumbika uliotungwa na mwimbaji mwenye sauti ya gharama Joseph Maina 'Big Maina' Ndani ya bendi ya OTTU Jazz (sasa Msondo Ngoma), wimbo unaanza na sauti za gharama za saksafoni na tarumbeta zilizopuliwa kwa umahiri mkubwa na Joseph Lusungu na Ramadhani Mnenge, hawa sasa wote ni marehemu pamoja na Maina mwenyewe Kwa upande wa tarumbeta Hamisi Mnyupe na Roman Mng'ande 'Romarii' wametamba wakicheza na tarumbeta zao. Katika video hii unayotazama ambayo siyo rasmi, unawaona Roman Mng'ande kushoto, katikati ni Ally Rashidi na kulia ni Hamis Mnyupe kushoto Sikiliza gitaa zito la bass ambalo lilipigwa na Suleiman Mwanyiro 'internet' na kwenye video hii unamuona mpiga bass Ibrahim Kandaya ambaye alikuja Msondo kwenye miaka ya 2000, kumbuka wimbo huu ni wa mwaka 1998. Joseph Maina, anayejulikana pia kwa jina la usanii kama "Mbunge wa Mkuzi", ndiye anatamba leo kwenye Sauti za gaharama na wimbo wake mahiri wa Chombo Kimeumbika. Josee Maina alikuwa mwimbaji na mtunzi mahiri na nguzo muhimu katika bendi kongwe ya muziki wa dansi nchini Tanzania, Msondo Ngoma Music Band, alikuwa na sauti ya gharama zilizotatiza na kuwateka wapenzi wa muziki wa dansi Wimbo wa "Chombo Kimeumbika" ulioachiwa mwaka 1998 na OTTU Jazz Band (sasa Msondo Ngoma) ni kazi maarufu ya Joseph Maina akiimba pamoja na TX Moshi William inayotumia sitiari ya "chombo" kusifu uzuri wa mwanamke. Unaelezea nia ya kuokoa "chombo" hicho kinachoelekea kuzama kutokana na manahodha wengi, huku wimbo huu ukiwa na sifa ya kuchochea matumizi ya neno "chombo" kumaanisha mwanamke mrembo nchini Tanzania. Ni hadithi tamu yenye mafundisho iliyofichwa na tafsida, lakini baya ni kwamba Josee Maina anaelezea namna alivyompenda msicha mrembo na kutaka kumwokoa na uhuni kwa kuwa wanaume wengi walikuwa wanamfuata lakini si kwa nia ya kuoa. Lakini Josee anashindwa na ushindani wa wanaume, anaona binti huyu akideti na wanaume mbalimbali, pamoja na uzuri na urembo wake wote, pamoja na nia nzuri ya Josee Maina kutaka kumwoa kumwokoa na umalaya, lakini anashindwa na kunyoosha mikono Matumizi ya neno Chombo kusadifu urembo wa mwanamke ama kumsifu kwa uzuri yalianza rasmi kutumiwa kwa kasi baada ya Wimbo Chombo Kimeumbika ulioimbwa kwa lugha fasaha na sanifu ya kiswahili yaani fasihi simulizi kwa tungo bora ya muziki wa dansi Joseph Maina alilifanya kazi kwa karibu na magwiji wengine kama TX Moshi William, Muhidin Maalim Gurumo, Suleiman Mbwembwe, Athumani Momba, Hassan Bitchuka, Hussein Jumbe nk. Joseph Maina alifariki dunia ghafla mnamo Februari 17, 2009, jijini Dar es Salaama, alifikwa na umauti akiwa ndani ya usafiri wa umma (daladala) lililokuwa likitokea Mwenge kuelekea Temeke akiwa amekaa mbele na dereva. Wakati huo alikuwa akitokea studio zilizoko Sinza kurekodi muziki .Ustawi wa mwili wake ulikatika ghafla akiwa amekaa kiti cha mbele, na abiria wenzake waligundua amepoteza maisha baada ya mwili wake kukakamaa. Inasikitisha sana Alikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Temeke ambapo madaktari walithibitisha kifo chake kabla ya kufikishwa hapo. Pamoja na kufariki kwake katika mazingira ya upweke na ya ghafla, urithi wa Joseph Maina bado unaishi. Nyimbo zake ukiwemo huu wa Chombo Kimeumbika, zinaendelea kupigwa kwenye redio na kumbi mbalimbali za burudani nchini Tanzania Joseph Maina anatajwa kama mmoja wa watu waliosaidia kulinda hadhi ya muziki wa dansi (Rumba ya Afrika Mashariki) dhidi ya ushindani wa muziki wa kizazi kipya. Tukirejea wimbo wa Chombo Kimeumbika, Ridhiwani Abdul Pangamawe 'Totoo' na vidole vyake vya gharama katika kupapasa nyuzi bin nyuzi, akiwa na mpini wa gitaa la solo, alitamba katika wimbo huu Alikuwepo Muhidin Maalim Gurumo 'Uncle' akiwa Kiongozi na nembo ya bendi wakati huo, alisimamia upangaji wa sauti (vocal arrangement) kuhakikisha muunganiko wa waimbaji hawa unaleta ladha halisi ya rumba. Wengine walioshiriki wimbo huo ni Saidi Mabera (gitaa la solo), Zahoro Bangwe (Rhythm), Suleimana Mwanyiro 'Internet' (Bass), Mnenge Ramadhani (saksafoni), Joseph Lusungu (saxfone), Hamisi Mnyupe (tarumpet), Romanus Mng'ande maarufu Romariii (tarumpeta) Joseph Maina 'Big Maina' ndiye sauti yetu ya gharama katika makala haya na Wimbo wake wa Chombo kimeumbika. Tukutane next time ..katika Makala haya ya Sauti za Gharama..ciao