TANZANIA NA BURUNDI KUANZA UJENZI WA RELI YA KISASA / TANZANIA NA BURUNDI KUANZA UJENZI WA SGR.
TANZANIA NA BURUNDI KUANZA UJENZI WA SGR. Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa na Rais wa Burundi Meja Jenerali Evariste Ndayishimiyiye, wameweka jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kisasa SGR ya kutoka Uvinza Kigoma Tanzania hadi Musongati nchini Burundi yenye urefu wa kilomita 240, ikiwa ni reli ya kwanza itakayounganisha nchi na nchi katika ukanda wa Afrika Mashariki. Akizungumza katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi uliofanyika eneo la Musongati, katika mkoa wa Buruga nchini Burundi, Waziri Mkuu ambaye amemwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, amesema utekelezaji wa mradi huo ni matunda ya ushirikiano baina ya nchi hizo ulioanzishwa mwaka 1975. Amesema kuwa mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa ajenda ya maendeleo ya nchi hizo na ajenda ya umoja wa Afrika ya mwaka 2063. Ameongeza kwamba mradi huo unalenga kuimarisha na kupanua miundombinu ya usafirishaji kati ya nchi hizo ili kurahisisha, kupunguza gharama na kuongeza ufanis wa shughuli za kibiashara na uhusiano uliopo wa wa kijamii baina ya nchi hizo na maeneo mengine ya ukanda wa Afrika wa Mashariki. Kwa upande wake, Rais wa Burundi, Meja Jenerali Evariste Ndayishimiye, amesema kuanza kwa ujenzi wa reli hiyo kutatibu shauku ya muda mrefu ya nchi hiyo kuwa na usafiri wa reli. Awali Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema kukamilika kwa ujenzi wa reli hiyo itaboresha maisha na uchumi wa wananchi wa pande zote mbili kwa kupunguza gharama za usafirishaji wa bidhaa kati ya Tanzania na Burundi. Hatua ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kisasa SGR kutoka Uvinza hadi Msongati, imewafurahisha wananchi wa pande zote mbili ambao wamesema itawaletea maendeleo.

Trump visits North Dakota flying aboard new Air Force One

Amakuru Ya BBC #iri Joro KAYUMBA NYAMWASA Arapfuye Nishyano

President Trump takes trip to North Dakota on new 'Air Force One' donated by Qatar

CIVIL WAR: GOP rebels DERAIL Trump's agenda as House shuts down

Pres. Trump talks SCOTUS rulings, Iran negotiations ahead of meeting in Doha

‘That’s the narrative Putin is trying to sell now’

US Decides Against Renewing USMCA, Shifting to Rolling Talks

Cargo ship runs aground in the Strait of Hormuz

Colorado's Melat Kiros poised to become first Gen Z member of Congress after primary win

Man Buys an Abandoned House and Restores It to New in 18 Months | by @The-Quinta

Supreme Court upholds birthright citizenship, allows trans athlete bans

House republicans TANK NDAA vote over SAVE America Act: It's a NONSTARTER! Lindsey Granger | RISING

DC fire chief warns of heat dangers before Fourth of July on National Mall

KTVB First Alert Extended Forecast: Heat builds into Fourth of July weekend
![UNITY FM 97.7 LIRA MORNING NEWS [01-07-2026]](https://i.ytimg.com/vi/8RpZcWSy3PA/hqdefault.jpg?sqp=-oaymwE9CNACELwBSFryq4qpAy8IARUAAAAAGAElAADIQj0AgKJDeAHwAQH4Af4JgALQBYoCDAgAEAEYTyBWKGUwDw==&rs=AOn4CLBuJzxMLoTIC-RtdkQXgSN1gIjOdg)
UNITY FM 97.7 LIRA MORNING NEWS [01-07-2026]

American pride falls to 25 year record low in new Gallup poll

Marcus Keupp: This Is How Russia Will Fall

