Mganga Mkuu wa Wilaya Dr Stanley Mlay akielezea huduma zitakazotolewa Zahanat

Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa Mhe.George N.Malima ameifungua rasmi Zahanati ya kijijj cha Iyoma iliopo Kata ya Gulwe Aprili 14,2026 ukishindikizwa na shamrashamra za Vifijo na furaha kutoka kwa Wananchi wa kijiji hicho. Zahanati hiyo iliyoanza kujengwa kwa nguvu za Wananchi na baadae walipokea kiasi cha Shilingi 60,000,000 kutoka Serikali kwa lengo la kumalizia boma la Zahabati hiyo Mhe Malima amewapongeza wananchi wa Iyoma kwa kupatiwa ufumbuzi wa kusogezewa huduma ya Afya karibu na kufutwa vilio vyao vya siku nyingi,pamoja na hayo amewataka kuitunza na kuienzi miundombinu ya Zahanati hiyo ili iweze kudumu na kutumika vizazi hadi vizazi. Nae, Mganga Mkuu wa Wilaya Dr. Stanley Mlay ameelezea huduma mbalimbali zitakazotolea na kupatikana ndani ya zahanati ikiwemo huduma ya magonjwa wa Nje ikiwa na maana ya magonjwa ya Malaria,U.T.I,Typhoid,Nimonia na magonjwa ya tumbo nakadhalika. Halikadhalika,huduma za Kliniki kwa mama wajawazito na watoto lakin pia amewasisitiza wamama wajawazito kuhudhuria kliniki mara tu wanapojigundua ni wajawazito wakiwa wameambatana na wenza wao ili wapate Elimu,pia huduma za vipimo vyote zitapatikana kikiwemo kipimo cha HIV/AIDS pamoja na huduma za chanjo kwa watoto. Dr Mlay amesema huduma za zahanati zitapatikana kwa masaa ishirini na nne kuanzia Aparili 15,2026 na kumshukuru Mgeni rasmi kwa muda wake aliojitoa kwa kufanikisha ufunguzi wa zahanati hiyo pamoja na timu nzima ya Halmashauri kufanikisha usimamizi mzuri wa ujenzi wa zahanati hadi kukamilika.