Mganga Mkuu wa Wilaya Dr Stanley Mlay akielezea huduma zitakazotolewa Zahanat
Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa Mhe.George N.Malima ameifungua rasmi Zahanati ya kijijj cha Iyoma iliopo Kata ya Gulwe Aprili 14,2026 ukishindikizwa na shamrashamra za Vifijo na furaha kutoka kwa Wananchi wa kijiji hicho. Zahanati hiyo iliyoanza kujengwa kwa nguvu za Wananchi na baadae walipokea kiasi cha Shilingi 60,000,000 kutoka Serikali kwa lengo la kumalizia boma la Zahabati hiyo Mhe Malima amewapongeza wananchi wa Iyoma kwa kupatiwa ufumbuzi wa kusogezewa huduma ya Afya karibu na kufutwa vilio vyao vya siku nyingi,pamoja na hayo amewataka kuitunza na kuienzi miundombinu ya Zahanati hiyo ili iweze kudumu na kutumika vizazi hadi vizazi. Nae, Mganga Mkuu wa Wilaya Dr. Stanley Mlay ameelezea huduma mbalimbali zitakazotolea na kupatikana ndani ya zahanati ikiwemo huduma ya magonjwa wa Nje ikiwa na maana ya magonjwa ya Malaria,U.T.I,Typhoid,Nimonia na magonjwa ya tumbo nakadhalika. Halikadhalika,huduma za Kliniki kwa mama wajawazito na watoto lakin pia amewasisitiza wamama wajawazito kuhudhuria kliniki mara tu wanapojigundua ni wajawazito wakiwa wameambatana na wenza wao ili wapate Elimu,pia huduma za vipimo vyote zitapatikana kikiwemo kipimo cha HIV/AIDS pamoja na huduma za chanjo kwa watoto. Dr Mlay amesema huduma za zahanati zitapatikana kwa masaa ishirini na nne kuanzia Aparili 15,2026 na kumshukuru Mgeni rasmi kwa muda wake aliojitoa kwa kufanikisha ufunguzi wa zahanati hiyo pamoja na timu nzima ya Halmashauri kufanikisha usimamizi mzuri wa ujenzi wa zahanati hadi kukamilika.

DC MAULID AAGIZA ENEO LA KIJIJI LILILOUZWA BILA IDHINI YA MKUTANO MKUU WA KIJIJI LIRUDISHWE

JESHI LA UHAMIAJI LATOA MAFUNZO KWA MAAFISA USAFIRISHAJI

ZAHANATI YA MSANGAMBUYA YAFUNGULIWA RASMI.

Focus JTA Sénégal : Sonko reprend le Pastef, Diomaye gouverne seul • FRANCE 24

DC MAULID DOTTO AAGIZA ENEO LA KIJIJI LILILOUZWA BILA IDHINI MKUTANO MKUU LIRUDISHWE

MAAFISA USAFIRISHAJI WATAKIWA KUFUATA UTARATIBU WA KUTUMIA VYOMBO VYA MOTO.

CGP MZEE AZINDUA ZAHANATI GEREZA KONGWA, AMEAHIDI KUENDELEA KUTEUA WAKUU WA MAGEREZA WANAWAKE.

KAMATI YA ALAT MKOA YAIPONGEZA MPWAPWA KWA MIRADI MIZURI.

DC MAULID DOTTO ALISHUKURU SHIRIKA LA COMPASSION KWA KUTOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO

MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA (PART 1)

JP Performance - Metal vs. Plastic! Which one gets stuck?!

VIJANA WAJASIRIA MALI WAPATIWA MAFUNZO YA UFUGAJI KUKU

30 May 2026

DC KONGWA ACHARUKA MBELE YA KIKAO "RAIS ALINICHAGUA, SIO JAMBO DOGO TUYAZINGATIE "

RC SENYAMULE ATOA POLE KWA WANAFUNZI WALIOUNGULIWA NA BWENI LA SEKONDARI MTERA

BILLION 30 KWENDA BADILISHA MAISHA MPWAPWA

MIILI YA ASKARI WALIOUAWA KWA KUPIGWA RISASI MPWAPWA YAAGWA

