Rais Magufuli atoa miezi 2 kwa TANESCO kupeleka umeme kiwanda cha kampuni ya Bakhresa Food Product.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametoa miezi miwili kwa shirika la umeme nchini TANESCO kuhakikisha umeme mkubwa wa uhakika unapatikana bila urasimu katika kiwanda cha kampuni ya Bakhresa Food Product kinachozalisha vinywaji baridi na kusindika matunda ili kumpunguzia gharama za uzalishaji.