MASKINI NUSU YA DARASA HAWAJUI KUSOMA NA KUANDIKA KATIKA SHULE YA MANDEPWENDE WILAYANI NAMTUMBO.

Shule ya msingi Mandepwende iliyopo wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma imebainika kuwa na wanafunzi 39 kati ya 89 wa darasa la saba wasiojua kusoma na kuandika . Hayo yamebainishwa na ANDERSONI MWALONGO ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ufutiliaji ya elimu iliyoundwa na katibu tawala mkoa wa Ruvuma juu ya matokeo mabaya ya darasa la saba na kidato cha nne kwa mwaka 2017 ambapo mkoa wa Ruvuma umefanya vibaya sana.