MACHIFU RUVUMA WAKANA KUMPA HECHE HADHI YA UCHIFU WA WANGONI
#habari Baada ya kusambaa mitandaoni habari za Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tanzania Bara, ndugu John Heche, kupewa cheo cha uchifu wa kabila la Wangoni, Baraza la Wazee wa Mila pamoja na Machifu wa Mkoa wa Ruvuma wamekanusha kuhusika na tukio la kumvisha vazi la uchifu. Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Baraza la Mila zilizopo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, Chifu Songea Mbano amezungumza kwa niaba ya Machifu wa mkoa wa Ruvuma, amesema kuwa wao kama machifu na wazee wa mila hawalitambui tukio la Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, ndugu John Heche, kuvalishwa mavazi ya kimila ya Kingoni tarehe 20 Juni 2026. Amesema kuwa tukio hilo lilifanywa na mwananchi mmoja, mcheza ngoma za asili anayefahamika kwa jina la Lusius Ponera, mkazi wa Mtaa wa Mshangano katika Manispaa ya Songea. Chifu Mbano ameeleza kuwa Ponera si chifu wala si mjumbe wa Baraza la Mila la Mkoa wa Ruvuma. Katika hatua nyingine, Chifu Songea Mbano amesema kuwa machifu wa Mkoa wa Ruvuma hawana mlengo wa chama chochote cha siasa na wanapinga mtu yeyote kuchukua jukumu au hadhi ya uchifu wakati si chifu halali. Aidha, amesema kuwa mtu hupewa hadhi ya uchifu kutokana na mchango wake kwa Taifa au kimataifa, na kwamba mchakato wa kumpatia hadhi hiyo lazima upitie Baraza la Machifu la Mkoa wa Ruvuma kwa mujibu wa taratibu za mila na desturi husika. #chivihimediaupdates

I Visited the African Country You've Never Heard Of 🇸🇹 (SĂŁo TomĂ© & PrĂncipe)

South Africa vs. Canada Highlights FIFA World Cup 2026 | Sportschau

Macron’s Humiliating Defeat: Burkina Faso Cuts All Ties, Accuses France of Backing Terrorists?

Heche Awatabiria Waliofanya Mauaji Oktoba 29 Kukutana na Yaliyomkumba Mnazi Hitler na Wafuasi Wake

MWALIMU ASIMULIA ALIVYOKATWA MKONO NA MUMEWE, WATOTO WAKE WAONE VIDOGOLE VILIVYOKATWA, WANAFUNZI

Israel's dream of ruling the region is over, its decline has begun | Mustafa Barghouti |UNAPOLOGETIC

Südafrika – Kanada Highlights Sechzehntelfinale, FIFA WM 2026 | sportstudio

MKEWE LISSU ASHINDWA KUZUIA MACHOZI AKIONGEA MBELE YA KAMATI YA HAKI ZA BINADAMU YA JUMUIYA YA ULAYA

SHUHUDIA MABORESHO MAKUBWA KWENYE UWANJA WA BOMA MASASI - MTWARA

SERIKALI YATOA SIKU 90 WAMILIKI KUSAJILI MAENEO YA KAZI OSHA

KUSUA SUA UTEKELEZAJI WA MIRADI KWAIBUA MJADALA BARAZA LA MADIWANI MTWARA MANISPAA

BIBI wa SUMBAWANGA amvaa WAZIRI MKUU MWIGULU kwa madai haya MAZITO "sitaki kiwanja nataka hela"

RC KUNENGE AZINDUA KIWANDA KIKUBWA CHA MAGODORO AFRIKA MASHARIKI

UCHAMBUZI MZITO KUHUSU AGIZO LA MARUFUKU MIKUTANO, JE HII INAMAANA GANI?

MTOTO WA ASKARI MAGEREZA ANYONGWA NA WASIOJULIKANA - MTWARA

TOUGH QUESTIONS FROM REPORTERS TO GERSON MSIGWA

Kolumbien – Portugal Highlights | Gruppe K, FIFA WM 2026 | sportstudio

PM MWIGULU responds to CHADEMA, speaks out on serious issues, uses the CONSTITUTION to clarify, a...

WAZIRI MAKONDA AWAVAA CHADEMA BUNGENI | WANAZUNGUKA KUKINANGA CHAMA CHA MAPINDUZI | SISI WAKUBWA

