MWELI AKARIBISHA UWEKEZAJI WA MATREKTA TANZANIA
#HABARI: Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli, ametembelea kiwanda cha kutengeneza matrekta cha MTW OJSC (Minsk Tractor Works) kilichopo katika Jamhuri ya Belarus, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi inayolenga kuimarisha ushirikiano wa kilimo na uwekezaji kati ya Tanzania na Belarus. Kiwanda hicho ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa matrekta na zana za kilimo, ikiwemo plau na haro, huku kikitengeneza matrekta yenye uwezo wa kuanzia farasi 15 hadi 500 kulingana na mahitaji ya wakulima wa ndani na wa kimataifa. Mbali na uzalishaji wa matrekta, kampuni hiyo hutoa huduma za matengenezo baada ya mauzo, mafunzo kwa waendeshaji na mafundi wa matrekta pamoja na ushauri kuhusu matumizi bora ya zana za kilimo ili kuongeza tija katika uzalishaji. Katika mazungumzo yake na uongozi wa kampuni hiyo, Bw. Mweli ameikaribisha MTW OJSC kuwekeza nchini Tanzania, akieleza kuwa nchi ina mazingira mazuri ya biashara na fursa kubwa ya soko kutokana na nafasi yake ya kimkakati ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Amesema uwekezaji wa kampuni hiyo nchini utasaidia kuongeza upatikanaji wa zana za kisasa za kilimo, kuchochea uzalishaji wa mazao, kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza ajira na kukuza mauzo ya mazao nje ya nchi. Bw. Mweli yuko nchini Belarus akimwakilisha Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, katika ziara ya kikazi inayolenga kuimarisha ushirikiano wa sekta ya kilimo kati ya Tanzania na Belarus, katika ziara hiyo, amepokelewa na Naibu Waziri wa Kilimo na Chakula wa Jamhuri ya Belarus, Mhe. Vitali Kulak.

Rais Samia wa Tanzania anatafuta nini Urusi? Katika Dira ya Dunia TV

🔴TAARIFA YA HABARI, SAA MBILI - JUNI 03, 2026 - UPATIKANAJI MBOLEA NCHINI TIMU YAUNDWA KUTATHMINI

🔴#LIVE: EXCLUSIVE: MCHUNGAJI MSIGWA AFICHUA MAZITO -SABABU KURUDI CHADEMA TUME ya CHANDE -CCM KWEMA?

BARABARA ZA MJINI ZNZ ZAANZA KUBOMOLEWA, UJENZI BARABARA ZA BILIONI 50.8 WAANZA

DON’T BUY A CHINESE CAR IF…

KOMBO AMVAA MBUNGE SIMAI ALIESEMA KUNA YUDA ANAMSALITI RAIS SAMIA/ ANACHONGANISHA VIONGOZI WETU HUYU

GPS: Bahrain and Kuwait felt the heat of IRAN's missile and drone attacks, the situation is volat...

When Tyson Faced the Smash Machine

Ũrĩmi wa ngũkũ cia broiler; #MũgamboWaMũrĩmi

Pakistani Man Uses 100yrs Old AMAZING TECHNIQUE To MAKE Ship Radiator

China Is Building East Africa's Largest Port in Tanzania

30 Real Life Superheroes | Random Acts of Kindness That Will Make You Cry #8

🔴TAARIFA YA HABARI YA ASUBUHI, JUNI 03, 2026: IMANI POTOFU KWA WAGONJWA WA KIFAFA KIKWAZO

TOO BAD: TEMA GPHA ROAD IS ALREADY FAILING Just 1year after constructing. How come?

MAZITO BODABODA ALIYEJIRUSHA CHINI YA LORI, "ALICHUKUA LAKI NANE"

How China Built an Impossible Bridge Above the Clouds

Things Are Not OK– Ndura Waruinge Raises Alarm Over Ruto|Plug Tv Kenya

Yurub ilaa Galbeedka Afrika - Ganacsatada Soomaaliyeed Waxay Isku Xireen Suuqyada Baabuurta Waaweyn

The $13 Billion Expressway China Built Across Algeria’s Harshest Terrain

