NITATEMBEA MBELE ZA BWANA

Composed by N.M Dancan Dominika ya Pili ya Kwaresma , ZABURI YA KUITIKIZANA (ZABURI 116:10 na 15, 16—17, 18—19 (K. 9) K. Nitatembea mbele za Bwana katika nchi za walio hai. Niliamini hata niliposema, "Mimi nimetaabika sana!" Kina thamani kubwa machoni pa Bwana kifo cha watakatifu wake. K. Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umevifungua vifungo vyangu. Nitakutolea dhabihu ya shukrani, na kuliita jina la Bwana. K. Nitamtimizia Bwana nadhiri zangu mbele ya watu wote, katika nyua za nyumba ya Bwana, ndani yako, ee Yerusalemu! K.