MKE WA MDUDE AELEZA MUMEWE ALIVYOTEKWA MBELA YAKE AKIWA NA MTOTO NA WALIOJITAMBULISHA NI POLISI
CHADEMA WASEMA JESHI LA POLISI LIMEHUSIKA UVAMIZI NYUMBANI KWA MDUDE, JESHI LA POLISI LAKANUSHA Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limekanusha taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii na zilizotolewa na baadhi ya viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA zinazodai askari polisi kuhusika na tukio la kuvamia, kuvunja mlango, kuingia ndani na kisha kumjeruhi Mpaluka Said Nyagali maarufu kwa jina la Mdude sehemu mbalimbali za mwili wake na kutoweka na mhanga na kwenda naye kusikojulikana. Taarifa ambayo imetolewa na kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kamishna msaidizi mwandamizi wa jeshi la polisi Benjamin Kuzaga imeeleza kuwa mnamo Mei 02, 2025 majira ya asubuhi, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilipokea taarifa kutoka kwa Sije Mbugi Emmanuel [31] mkazi wa Iwambi ambaye ni mke wa Mpaluka Said Nyagali maarufu kwa jina la Mdude kuwa mnamo Mei 02, 2025 majira ya saa 08:00 usiku wakiwa wamelala huko Mtaa wa Ivanga, Kata ya Iwambi Jijini Mbeya watu wasiofahamika waliwavamia baada ya kuvunja mlango na kuingia ndani na kisha kumjeruhi Mpaluka Said Nyagali na kufanikiwa kutoweka na mhanga na kwenda naye kusikojulikana. Mapema hii leo akizungumza na wanabari mke wa Mpaluka Said Nyagali maarufu kwa jina la Mdude, Sije Mbugi Emmanuel [31] amewaomba wanahabari kumsaidia kupaza sauti ili mume wake apatikane huku akilituhumu jeshi la polisi kuhusika na uvamizi huo. Abdukarim Juma ni rafiki wa Mpaluka Said Nyagali maarufu kwa jina la Mdude yeye anaeleza namna ambavyo alipata taarifa na hatua alizozichukua. Viongozi mbalimbali wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Taifa, kanda ya Nyasa na mkoa wa Mbeya wamelaani tukio hilo huku wakilitupia lawama jeshi la polisi. Mpaluka Said Nyagali maarufu kwa jina la Mdude ni mwanaharakati na mwanachama chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA ambaye majira ya saa 08:00 usiku akiwa amelala huko Mtaa wa Ivanga, Kata ya Iwambi Jijini Mbeya watu wasiofahamika waliwavamia baada ya kuvunja mlango na kuingia ndani na kisha kumjeruhi Mpaluka Said Nyagali na kufanikiwa kutoweka na mhanga na kwenda naye kusikojulikana.

BALOZI AUWAWA KWA KUCHOMWA VISU ZAIDI YA 10 NDUGU WADAI HAKUWA NA UGOMVI NA MTU YEYOTE.

MTOTO WA MIAKA MIWILI ANAYE TREND KWA MISEMO YA "NASOMA VETA LA KUMI, MJOMBA NI MAMA"

MANENO YA MDUDE KABLA YA KUKAMATWA.

MKE WA MDUDE AMWAGA MACHOZI AKIELEZA WALIOJIITA POLISI WALIVYOVAMIA NYUMBANI KWAO NA KUMCHUKUA MDUDE

MKE WA MDUDE AFUNGUKA MUMEWE ALIVYOTEKWA

MDUDE AKIELEZA YALIYO MSIBU AKIWA MIKONONI MWA POLISI

MAJIBU YA TULIA KUPOTEA KWA MDUDE, UTEKAJI NA WATU WASIOJULIKANA

How Kenya Can Lower Fuel Prices | Ndindi Nyoro

AMATEKA Y'URUGAMBA,Lt Gen KARENZI Karake,Gen IBINGIRA,Maj Gen Sam KAKA,Col Dodo,bacyuye igihe,bumve

#Tanzania : Mdude Nyangali afunguka (Part 2)

WANAHARAKATI WAIBUA SIRI MASENETA WA MAREKANI KUIWEKEA BURN VISA ZA WANACCM, WABUNGE(BULAYA,KAMBO)

A FRIEND MENTIONS MBOWE - "HE'S SLEEPING WITH HIS WIFE, I'VE BEEN POLITICALLY CAPTURED"

🔴LIVE:WAKILI MADELEKA ANAUNGURUMA MUDA HUU,ANAFUNGUKA MAZITO

LATIFA AOMBA MSAMAHA KWA MPENZI WAKE ALIYEMJERUHI KWA KUTUMIA KISU "TULIKUWA TUMELEWA WOTE"

Gachagua: I WILL CALL MAANDAMANO IF RUTO DOESN'T STOP GRABBING IMENTI FOREST. SHAME ON YOU KINDIKI

BABA LEVO BUNGENI AWASHUGHULIKIA WANAWAKE WANAOKULA NAULI ZA WANAUME " WANALETE KIBURI"

MBUNGE SIGRADA MLIGO AFUNGUKA SUALA LA LUPIGWA TAARIFA BUNGENI LEO.

CHADEMA WAFUNGUKA MWANZO MWISHO TUKIO ZIMA LA UPOTEAJI WA MDUDE

AVAMIWA KWAKE NA KUCHUKULIWA PIKIPIKI ,GODORO NA KITANDA KKISA DENI LA SHILINGI LAKI 2 NA ELFU 15.

