AMCHAYE BWANA BY A.I.C DAGORETTI CORNER - TUMAINI CHOIR

Zaburi 112 1 Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake. 2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa. 3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele. 4 Nuru huwazukia wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki. 5 Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki. 6 Kwa maana hataondoshwa kamwe; Mwenye haki atakumbukwa milele. 7 Hataogopa habari mbaya; Moyo wake u imara ukimtumaini BWANA. 8 Moyo wake umethibitika hataogopa, Hata awaone watesi wake wameshindwa.