ODM yamtimua tena Sifuna kama Katibu Mkuu

Kwa mara ya pili ODM kimemtimua Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna kama katibu mkuu wa chama hicho. Uamuzi huu uliafikiwa baada ya kikao cha kamati kuu ya ODM chini ya kinara Oburu Oginga kilichoidhinisha maamuzi ya kamati ya kutatua migogoro ya chama. Uamuzi wa kumtimua Sifuna unajiri siku mbili baada ya jopo la kutatua migogoro ya kisiasa kuagiza ODM kuanzisha tena mchakato wa kumwondoa.