"MHE. HEMED ZANZIBAR YAENDELEA KUIIMARISHA YA SHERIA, YAWEKEZA BILIONI 13.6 KATIKA HAKI NA MAHAKAMA"

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatambua na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka hasa katika usimamizi wa haki jinai, Utawala wa sheria na ulinzi wa maslahi ya umma. Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt Hussein Ali Mwinyi katika Maadhimisho ya Miaka 24 tokea kuanzishwa kwa Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar yaliyofanyika katika ukumbi wa Madinatul Bahari Mbweni Zanzibar. Amesema uwepo wa Afisi Mkurugenzi wa Mashtaka kumesidia kuimarika kwa utawala wa sheria ambao unatoa mgawanyo sahihi wa madaraka na majukumu kati ya taasisi mbali mbali za haki jinai. Mhe. Hemed amesema mfumo wa haki jinai umekuwa ni nguzo muhimu ya kulinda haki za wananchi, kuimarisha imani ya jamii kwa taasisi za dola na kujenga mazingira salama ya uwekezaji na maendeleo ya kiuchumi. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amefahamisha kuwa mfumo huo unatoa mchango mkubwa katika mapambano dhidi ya uhalifu wa aina mbalimbali ikiwemo rushwa, dawa za kulevya, uhalifu wa kimtandao, uhujumu uchumi, utakatishaji wa fedha haramu pamoja na vitendo vya ukatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto, hivyo Serikali itaendelea kuziimarisha taasisi zake ili ziweze kukabiliana ipasavyo na changamoto hizo zinazobadilika siku hadi siku. Aidha Mhea Hemed amasema Serikali itaendelea kuipa kipaombele sekta ya sheria na haki ili kufikia malengo ya Dira ya maendeleo ya Zanzibar ya 2050 sambamba na kuweka mkazo katika kujenga taasisi zenye uwezo, kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma za sheria na haki ambapo serikali imeweka zaidi ya Bilioni 13.6 kwa ajili ya kuimarisha majengo ya mahakama, miundombinu ya TEHAMA pamoja na vitendea kazi ili kurahisisha wananchi kupata haki zao kwa wakati na kwa usawa. Amesema katika kuongeza ufanisi wa kazi, serikali imeboresha maslahi ya wafanyakazi, kuimarisha mazingira ya kazi na kuwekeza katika matumizi ya teknolojia ya kisasa, kuwajengea uwezo waendesha mashtaka na wapelelezi kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo. Sambamba na hayo Mhe. Hemed amewahimiza viongozi na watumishi wa sekta ya sheria na haki kuwekeza katika maarifa, ubunifu na matumizi ya mifumo ya kisasa na kuendelea ili kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, uzalendo, weledi na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma. Hata hivyo, ametoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa za uhalifu, kushiriki katika utoaji wa ushahidi pale inapohitajika na kuendelea kuwa walinzi wa amani na utulivu na kuendelea kuijenga zanzibar yenye haki, amani, utawala bora na maendeleo endelevu kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo. Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala bora Mhe. Dkt. HAROUN ALI SULEIMAN amesema Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka imekuwa ikifanya kazi kubwa hasa katika kusimamia upatikanaji wa haki jambo lililoleta mabadiliko makubwa na kuwajengea Imani kwa wananchi juu ya upatikanaji wa haki zao katika vyombo vya sheria. Waziri Dkt. HAROUN ameitaka Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kufanya kazi kwa kushirikiana na Mamlaka ya kuzuia rushwa na uhujumu uchumi pamoja na Kamisheni ya kupambana na Madawa ta kulevya ili kuondoa mianya yote ya rushwa, ubadhirifu wa mali za Umma na mianya yote ya rushwa Kwa upande wake Mkurugezi wa Mashtaka Zanzibar Mhe. MGENI JECHA JAILANI amesema katika kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi, Katiba ya Zanzibar inamuelekeza Mkurugenzi wa Mashtaka kutekeleza majukumu yake kwa kuhakikisha kwamba haki inatendeka, maslahi ya umma yanalindwa na matumizi mabaya ya vyombo vya sheria yanaepukwa. Mhe. JAILANI amesema Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka imepiga hatua kubwa katika kinpindi cha Uongozi wa Awamu ya Nane ( 8 ) ikiwemo kufanyiwa marekebisho ya sheria mbali mbali zinazohusu haki jinai, kuimarika kwa ushirikiano na Taasisi za haki jinai na kuwepo kwa mageuzi ya kidijitali katika utoaji wa huduma za Mashtaka. Aidha, Mhe. Jailani amesema licha ya mafanikio hayo, Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka inakabaliwa na changamoto ya uhaba na uchakavu wa majengo na vipando vya Ofisi pamoja na maslahi ya waendesha mashtaka ili yaendane na uzito wa majukumu wanayoyatekeleza.

KUMEKUCHA ZANZIBAR YAIMARISHA VITA DHIDI YA RUSHWA, ZAIDI YA BILIONI 5 ZAOKOLEWA
▶︎

KUMEKUCHA ZANZIBAR YAIMARISHA VITA DHIDI YA RUSHWA, ZAIDI YA BILIONI 5 ZAOKOLEWA

The Most Important Country in Africa You’ve Never Heard Of (Djibouti 🇩🇯)
▶︎

The Most Important Country in Africa You’ve Never Heard Of (Djibouti 🇩🇯)

OMO ATOA DARASA MBELE YA RAIS MWINYI NA DKT SAMIA HII NI HISTORIA KWA UPINZANI
▶︎

OMO ATOA DARASA MBELE YA RAIS MWINYI NA DKT SAMIA HII NI HISTORIA KWA UPINZANI

Heated Debate on the Future of Reconciliation in Zanzibar | DW ROUND TABLE
▶︎

Heated Debate on the Future of Reconciliation in Zanzibar | DW ROUND TABLE

WATCH: Kate and William Attend Wimbledon 2026 Men’s Final
▶︎

WATCH: Kate and William Attend Wimbledon 2026 Men’s Final

Zanzibar Travel Guide  | Best Beaches, Hotels, Things to Do
▶︎

Zanzibar Travel Guide | Best Beaches, Hotels, Things to Do

Amazing Toilet Bowl Manufacturing Process | How Toilet Bowls Are Made in Factory
▶︎

Amazing Toilet Bowl Manufacturing Process | How Toilet Bowls Are Made in Factory

I Repaired the Broken Swing Gear which no Mechanic Repairs |Give your Opinion by Watching the Video
▶︎

I Repaired the Broken Swing Gear which no Mechanic Repairs |Give your Opinion by Watching the Video

Afghan most Famous Kabuli Pulao | Pakistani Karahi | Biryani recipe | Roasted chicken | Street food
▶︎

Afghan most Famous Kabuli Pulao | Pakistani Karahi | Biryani recipe | Roasted chicken | Street food

🔴#Live:MAMA FATMA AIBIWA PESA YA NAULI! MASWALI MAGUMU KUHUSU AJENT,MKATABA NA HAKI ZA WAFANYAKAZI..
▶︎

🔴#Live:MAMA FATMA AIBIWA PESA YA NAULI! MASWALI MAGUMU KUHUSU AJENT,MKATABA NA HAKI ZA WAFANYAKAZI..

Rais Mwinyi leo amtumbua Mkurugenzi wa ZRB
▶︎

Rais Mwinyi leo amtumbua Mkurugenzi wa ZRB

DKT. SAADA : ZANZIBAR HAIWEZI KUBEBA MATIBABU YA WATU MILIONI 60, KAULI YANGU IMEPOKELEWA KISIASA
▶︎

DKT. SAADA : ZANZIBAR HAIWEZI KUBEBA MATIBABU YA WATU MILIONI 60, KAULI YANGU IMEPOKELEWA KISIASA

Samia vs The West: The REAL POWER PLAY Behind Tanzania's Protest
▶︎

Samia vs The West: The REAL POWER PLAY Behind Tanzania's Protest

SEREKALI YADHIBITI UCHAFU FORODHANI
▶︎

SEREKALI YADHIBITI UCHAFU FORODHANI

Man Uses FREE ABANDONED PALLETS to Build a House in the Forest | Full Build by @lesnoy
▶︎

Man Uses FREE ABANDONED PALLETS to Build a House in the Forest | Full Build by @lesnoy

A shocking find in stump in a cemetery
▶︎

A shocking find in stump in a cemetery

Aliko Dangote’s $46B Warning to Africa: Industrialize or Remain Left Behind!
▶︎

Aliko Dangote’s $46B Warning to Africa: Industrialize or Remain Left Behind!

US launches new wave of airstrikes on Iran
▶︎

US launches new wave of airstrikes on Iran

MAADHIMISHO YA SIKU YA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA BARANI AFRIKA- 2026
▶︎

MAADHIMISHO YA SIKU YA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA BARANI AFRIKA- 2026

Secretary  Marco Rubio Unveils NEW U.S. "Patriot Passport" – Huge Changes Coming!
▶︎

Secretary Marco Rubio Unveils NEW U.S. "Patriot Passport" – Huge Changes Coming!