Balozi wa Tanzania nchini India afafanua sakata la binti aliyedaiwa kufukuzwa ubalozini
Ubalozi wa Tanzania nchini India umetoa ufafanuzi kuhusu Mtanzania, Sayuni Eliakim aliyedaiwa kushindwa kusaidiwa ubalozini hapo kupata hati ya kusafiria ili arudi Tanzania. Ubalozi huo umetoa ufafanuzi ikiwa ni siku mbili tangu taarifa hizo zilizodai Sayuni aliyedaiwa kunyanyang’anywa hati ya kusafiria na mwenyeji wake kuwa alikosa huduma ubalozini hapo na kumtaka arudi ajaze maombi hayo kwa njia ya mtandao. Ufafanuzi huo umetolewa leo Jumatatu Agosti 28, 2023 na Balozi wa Tanzania nchini humo, Anisa Mbega ambaye amesema kuwa Sayuni alizidisha muda wa kibali chake cha ukaazi nchini humo, hivyo kuna ugumu katika mchakato wa kumrudisha Tanzania. “Sayuni Eliakim aliingia nchini India mwaka 2018, na kukaa kwa muda mrefu hadi kujikuta muda wake wa ukaazi umepita. Kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za uhamiaji za India, raia wa kigeni ambaye amepitisha muda wake wa ukaazi, haruhusiwi kutoka nchini India, isipokuwa kwa utaratibu maalum uliowekwa. “Utaratibu huo ni pamoja na kuomba ruhusa ya kutoka nje ya nchi (Exit Permit). Maombi ya ‘Exit Permit’ yanatakiwa kufanyika katika mji ambao mhusika anaishi (kwa upande wa Sayuni mji anaoishi ni Bangalore). Sayuni alielekezwa kuhusu utaratibu huo na maombi yake hadi hivi sasa yanaendelea kufanyiwa kazi,”amesema Balozi Anisa. Balozi Anisa amesema wanaendelea kumsaidia Sayuni kwa kumpatia Hati ya kusafiria ya dharura (ETD). Aidha, Ubalozi umetoa rai kwa Watanzania kujiepusha na kuchukua tahadhari na watu wasio waaminifu wanaowalaghai kuhusu kuwepo kwa nafasi za ajira zisizo na ujuzi kwa raia wa Tanzania nchini India.

MTANZANIA ALIYE FUNGWA MIAKA 10 NCHINI IRAN ASIMULIA MAZITO / VIFO SINDANO YA SUMU /PART 1

Wasichana wakitanzania kujikuta wakitumikishwa katika biashara ya ngono India

KUTOKA INDIA: MUNA AFICHUA MATESO WANAYOPITIA MABINTI wa KITANZANIA INDIA - "TUNAYANG'ANYWA PASPOTI"

PART 1: KABLA YA KUOKOKA, MREMBO AFICHUA ALIVYOISHI INDIA KWA KUDANGA na KUNUSURIKA KUFA KWA UKIMWI

MTANZANIA ANAYEDAI MUMEWE KUPANGA KUMUUA, BALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA WATOA TAMKO HILI

BALOZI WA MAREKANI NCHINI TANZANIA ALIVYOZINDUA OFFICE YA REMAX COASTAL YA KIMAREKANI

Watanzania waishio India, Wasamehewa Faini ya kuondoka India. Wapewa Maelekezo

AMKA NA BBC KISWAHILI LEO JUMATATU/22)6/2025

#EXCLUSIVE: JIYA -''MIMI SIYO RAIA wa INDIA ni MTANZANIA NINAKITAMBULISHO -NIMEPATA BAHATI KUIGIZA''

Inside Little Mogadishu in Uganda, Somali city away from Somalia 🇸🇴

MPINA AJIBU WABUNGE WALIOSEMA WATAKWENDA KUMSHTAKI KWENYE VIKAO NEC "CCM SIO PANGO LA WALANGUZI"

VILIO VYATAWALA MWILI wa MREMBO wa KITANZANIA ALIYEFARIKI INDIA UKIWASILI TANZANIA KWA MAZIKO

India Most Dangerous Slum 🇮🇳

MSUKUMA AMTOLEA UVIVU MARTHA KARUA MWANAHARAKATI WA KENYA AMTAKA AACHANE NA SIASA ZA TANZANIA

#live RAIS SAMIA AKIMPOKEA RAIS NETUMBO NANDI-NDAITWAH, IKULU DAR ES SALAAM JUNI 20, 2026

Mazungumzo na Mama Anna Tibaijuka: Oktoba 29 | Sakata la Yuda |Tanganyika-Zanzibar| Kesi Tundu Lissu

MWANZO HABARI LIVE: Balaa! Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania wafungwa!

MTANZANIA AKWAMA INDIA - AFUNGIWA KAMBINI - BILA MIL 3 HAWEZI KURUDI - MAMA'AKE AOMBA MSAADA...

TAKRIBANI WANAFUNZI 100 WAMEONDOKA KWENDA NCHINI INDIA KUPITIA KAMPUNI YA GLOBAL EDUCATION LINK

