🔴#BREAKING: MAPAPA wa DAWA za KULEVYA WAKAMATWA KIGAMBONI -WANATAFUTWA DUNIANI KOTE - "KILO 3,182"..

🔴#BREAKING: MAPAPA wa DAWA za KULEVYA WAKAMATWA KIGAMBONI -WANATAFUTWA DUNIANI KOTE - "KILO 3,182".. Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya Tanzania (DCEA) imekamata jumla ya kilogramu 3,182 za dawa za kulevya aina ya heroin na methamphetamine katika operesheni maalum iliyofanyika jijini Dar es Salaam na Iringa kati ya tarehe 5 hadi 23 mwezi Disemba, 2023. Watu saba wamekamatwa kuhusika na dawa hizo ambapo wawili kati yao wana asili ya Asia. Kiasi hiki cha dawa za kulevya kinajumuisha kilogramu 2,180.29 za dawa aina ya methamphetamine na kilogramu 1001.71 aina ya heroin zilizokamatwa katika wilaya za Kigamboni, Ubungo na Kinondoni jijini Dar es Salaam pamoja na wilaya ya Iringa mkoani Iringa. Ukamataji huu umehusisha kiasi kikubwa cha dawa za kulevya ambacho hakijawahi kukamatwa katika historia ya Tanzania tangu kuanza kwa shughuli za udhibiti wa dawa za kulevya. Hivyo, watuhumiwa waliokamatwa ni miongoni mwa mitandao mikubwa ya wauzaji wa dawa za kulevya inayofuatiliwa nchini na duniani. Aidha, dawa hizi zilizozikamata zilikuwa zimefungashwa kwenye vifungashio vya bidhaa zenye chapa mbalimbali za kahawa na majani ya chai. Mbinu hii inatumika kwa lengo la kurahisisha usafirishaji wake na kukwepa kubainika. Ukiacha dawa ya heroin inayotengenezwa kwa mchanganyiko wa kemikali kutoka kwenye mimea ya afyuni (opium popy) inayolimwa katika nchi za Asia na baadhi ya kutoka Amerika, dawa aina ya methamphetamine ni dawa mpya ya kulevya iliyopo katika kundi la vichangamshi sawa na cocaine. Dawa hii huwa kwenye mfumo wa vidonge, unga au chembechembe mithili ya chumvi ang’avu yenye rangi mbalimbali ambayo huzalishwa kwenye maabara bubu kwa kuchanganya aina mbalimbali za kemikali bashirifu. Dawa hii ni hatari kwa afya ya mtumiaji, madhara yake ni makubwa na hayatibiti kirahisi kwani mtumiaji hupata madhara ya kudumu kwenye ubongo na hivyo hupunguza uwezo wa kutunza kumbukumbu, kusababisha uraibu na kuathiri mfumo mzima wa fahamu. Kiasi cha dawa za kulevya zilizokamatwa, endapo zingefanikiwa kuingia mtaani zingeweza kuathiri zaidi ya watu 76,368,000 kwa siku. Hivyo, ukamataji huu umeokoa nguvu kazi ambayo ingeangamia kutokana na madhara yatokanayo na matumizi ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi. Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa a Kulevya, inatoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Mamlaka kwani mafanikio haya yametokana na ushirikiano unaotokana na wananchi wanaotoa taarifa juu ya watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya ikiwa ni pamoja na weledi na uzalendo mkubwa wa maafisa wa Mamlaka katika udhibiti wa biashara ya dawa za kulevya. Pia, Mamlaka inatoa onyo kwa wote wanaoendelea kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya hapa nchini kuacha badala yake wajikite kwenye biashara nyingine halali kwani Mamlaka imejizatiti kukomesha biashara ya dawa za kulevya kwa kufanya operesheni katika maeneo mbalimbali nchini. Aidha,Mamlaka inaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha Mamlaka katika kutekeleza kazi zake kwa ufanisi mkubwa. Tukishirikiana, kwa umoja wetu tutaweza kuokoa vizazi vyetu na taifa letu dhidi ya tatizo la dawa za kulevya. ⚫️ JE, NA WEWE UNA HABARI? ⚫️ WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE: ( +255 739 750910), ( +255 783453136) ⚫️ Email: [email protected] ⚫️ OUR PLAYLISTS: ⚫️ MICHEZO na BURUDANI:    • Habari zote za michezo na Burudani Tanzania!   ⚫️ HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA: http://bit.ly/mikasa_ya_kusisimua ⚫️ GLOBAL RADIO TV: http://bit.ly/255globalradio ⚫️ EXCLUSIVE INTERVIEW: http://bit.ly/exclusive_interviews ⚫️ SIKILIZA + 255 GLOBAL RADIO LIVE: http://ndstream.net/globalradio/ ⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

The Story Book : Ukweli Uliojificha Kuhusu BANGI
▶︎

The Story Book : Ukweli Uliojificha Kuhusu BANGI

Yusuph Manji baada ya kutajwa na Makonda sakata la dawa za kulevya
▶︎

Yusuph Manji baada ya kutajwa na Makonda sakata la dawa za kulevya

DOCUMENTAR RECORDER. În interiorul sectei lui Pomohaci
▶︎

DOCUMENTAR RECORDER. În interiorul sectei lui Pomohaci

GWIJI WA KUUZA DAWA ZA KULEVYA ADAKWA KAMISHNA JENERALI AFUNGUKA MAZITO/ ANAMTANDAO DUNIA NZIMA
▶︎

GWIJI WA KUUZA DAWA ZA KULEVYA ADAKWA KAMISHNA JENERALI AFUNGUKA MAZITO/ ANAMTANDAO DUNIA NZIMA

RAIA WA PAKISTAN WALIVYONASWA NA DAWA ZA KULEVYA KATIKA JAHAZI "TUMEWAPELEKA MAHAKAMANI"
▶︎

RAIA WA PAKISTAN WALIVYONASWA NA DAWA ZA KULEVYA KATIKA JAHAZI "TUMEWAPELEKA MAHAKAMANI"

Kiwewe cha ‘polygamist’: Je wanawake wengi wanaezapenda mume mmoja kwenye ndoa | Gumzo La Sato
▶︎

Kiwewe cha ‘polygamist’: Je wanawake wengi wanaezapenda mume mmoja kwenye ndoa | Gumzo La Sato

HAMIS KIGGUNDU: BILIONEA MDOGO MWENYE UTAJIRI WA KUTISHA ALIYEANZIA KUUZA MITUMBA | THE BRAIN FOOD
▶︎

HAMIS KIGGUNDU: BILIONEA MDOGO MWENYE UTAJIRI WA KUTISHA ALIYEANZIA KUUZA MITUMBA | THE BRAIN FOOD

THE BRAIN FOOD: KIM KIDUKU; MKOREA MBABE WA MAKOMBORA YA NYUKLIA YANAYOITIKISA MAREKANI...
▶︎

THE BRAIN FOOD: KIM KIDUKU; MKOREA MBABE WA MAKOMBORA YA NYUKLIA YANAYOITIKISA MAREKANI...

Mambo ya kutegemea ukikaa ukweni
▶︎

Mambo ya kutegemea ukikaa ukweni

🔴#Live: MAUMIVU BASI! MWAKA MMOJA wa MARIDHIANO CCM na CHADEMA / MARUFUKU ya NGUO za MITUMBA GUMZO..
▶︎

🔴#Live: MAUMIVU BASI! MWAKA MMOJA wa MARIDHIANO CCM na CHADEMA / MARUFUKU ya NGUO za MITUMBA GUMZO..

KILOGRAMU  798.893 ZA DAWA ZA KULEVYA ZAKAMATWA ZANZIBAR OCT-DEC 2024, SHISHA ZATAJWA PIA
▶︎

KILOGRAMU 798.893 ZA DAWA ZA KULEVYA ZAKAMATWA ZANZIBAR OCT-DEC 2024, SHISHA ZATAJWA PIA

🔴DIRECT | PENCOO avec Moustapha Diop et son équipe de ce Vendredi 04 AVRIL 2025
▶︎

🔴DIRECT | PENCOO avec Moustapha Diop et son équipe de ce Vendredi 04 AVRIL 2025

Gor vs Ingwe: Inside the Mashemeji Derby rivalry in Kenya, rituals and myths
▶︎

Gor vs Ingwe: Inside the Mashemeji Derby rivalry in Kenya, rituals and myths

I'M WARNING DCI & HAVE SUMMONED IG KANJA IN COURT! Babu Owino fumes in court over GenZ abductions
▶︎

I'M WARNING DCI & HAVE SUMMONED IG KANJA IN COURT! Babu Owino fumes in court over GenZ abductions

Fahamu vipengele vyenye ukakasi Sheria ya Usalama wa Taifa
▶︎

Fahamu vipengele vyenye ukakasi Sheria ya Usalama wa Taifa

ISHU ya JOSHUA KUWA MWANAJESHI wa ISRAEL -BABA YAKE KWENDA ISRAEL: FAMILIA YATAKA SERIKALI IELEZE...
▶︎

ISHU ya JOSHUA KUWA MWANAJESHI wa ISRAEL -BABA YAKE KWENDA ISRAEL: FAMILIA YATAKA SERIKALI IELEZE...

'I Warn You - Don't Provoke Russia': Jeffrey Sachs ROARS At EU & US In European Parliament | VIRAL
▶︎

'I Warn You - Don't Provoke Russia': Jeffrey Sachs ROARS At EU & US In European Parliament | VIRAL

Pencoo de ce Vendredi 09 Mai 2025 avec Moustapha Diop et sa Team Invité DAME MBODJ  Sur WalfNet
▶︎

Pencoo de ce Vendredi 09 Mai 2025 avec Moustapha Diop et sa Team Invité DAME MBODJ Sur WalfNet

Abductions Are Back; Nairobi Is The Epicentre | Eugene Wamalwa
▶︎

Abductions Are Back; Nairobi Is The Epicentre | Eugene Wamalwa

HECHE: MKE WA TUNDU LISSU NA DADA YAKE POLE POLE WAMEUWASHA MOTO BUNGE LA ULAYA
▶︎

HECHE: MKE WA TUNDU LISSU NA DADA YAKE POLE POLE WAMEUWASHA MOTO BUNGE LA ULAYA