HAMZA MZEE PART 159

Baada ya kusubiri kwa muda mchache tu, palepale aliweza kuona mtu akipanda kwenye shimo hilo. Mtu huyo alikuwa mwembamba mno na mikono mirefu na mweusi. Usoni alikuwa na ndevu ndefu kama rasta. Licha ya kwamba alikuwa na hali ya weusi wa ngozi, lakini nywele zake ni kama zimebadilika kutoka kuwa katika hali ya weusi na kuwa kijani. Kwa lugha nyepesi mtu huyu alikuwa tofauti sana na wale wamanjano Hamza aliokabiliana nao kipindi kile. Instagram: @lucaslumbasi_tz #simulizi #truestory #simulizizalumbasi