Kazi yangu ikiisha | When my Life-work is Ended | Nyimbo za Kristo

Lyrics 1. Kazi yangu ikisha, nami, nakiokoka, Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi; nivukapo ng’amboni Atakuwa wa kwanza kunilaki. Nitamjua, nitamjua, Nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, Kwa alama za misumari. 2. Kuona uso wake utanipa furaha, Furaha isiyo ya kukomesha; Nitamsifu Mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyo nipa pahali mbingini. 3. Nao walio kufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza. 4. Milangoni mwa mji Bwana atanipisha, Pasipo machozi awla huzuni. Nitauimba wimbo wa milele: lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.