Wakulima wa Zao la Tumbaku Chunya na Songwe Wanufaika na Msaada Kutoka Premium Active Tanzania

#Chunya Kampuni ya Premium Active Tanzania imekabidhi msaada wa Shilingi Milioni Arobaini na Saba na Laki Nane (47,800,000/=) kwa wakulima wa zao la tumbaku kwa kata Saba katika wilaya za Chunya na Songwe ili kuinua sekta ya kilimo Cha zao hilo. Hayo yameelezwa na meneja Niko layssos wakati akiwasiliaha taarifa kwa mgeni wa heshimamkuu wa Wilaya ya chunya saimoni Mayeka ambapo amesema lengo lao ni kuhakikisha wanaisaidia jamii kutatua changamoto Mmoja wa wakulima wa zao Hilo la tumbaku ameishukuru Serikali kwa namna wanavyotatua changamoto mbalimbali za wakulima huku akiendelea kwa kumshukuru kampuni ya primia kwa kuwajali wakulima Kwa niaba ya madiwani diwani nikson mwankuga ameishukuru campuni ya primia kwa kuendelea kuwasaidia wakulima katika maeneo Yao kwani wamekuwa msaada mkubwa katika kukuza sekta hiyo ya kilimo Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya chunya saimoni Mayeka ambaye ndiye mgeni wa heshima kwenye hafla hiyo amesema pamoja na changamoto zilizopo kwenye kilimo lakini Bado wakulima na makampuni wamesimamia vizuri msimu huu wa kilimo na hivyo kuleta wameyaona matunda katika kuzalisha zao Hilo Aidha DC Anasema wao kama Serikali ni kuhakikisha wanawawekea wakulima mazingira Rafiki ili waweze kuona tija kwenye kilimo Chao na kwamba wataendelea kuwasaidia wakulima ili wawezi kuzalisha mazao yao kwa wingi.