WANANCHI TUNDURU NA NACHINGWEA WAOMBA KUJENGEWA DARAJA MTO LUMESULE

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Ngapa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma pamoja na wananchi wa Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi, wameiomba serikali kuwajengea daraja katika mto Lumesule unaounganisha wilaya hizo, ili waweze kuondokana na adha wanazozipata hasa kipindi cha mvua ikiwa ni pamoja na kukuza zaidi biashara zao.