IEBC yatishia kuahirisha uchaguzi mdogo wa Ol-Kalou
Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka, IEBC, imetishia kuahirisha uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Ol-Kalou ulioratibiwa kufanyika Alhamisi ijayo. Hatua hiyo inafuatia ripoti za vurugu na madai ya uhongaji wa wapiga kura katika kampeni zinazoendelea eneo hilo. Akizungumza jijini Nairobi leo, Mwenyekiti wa IEBC, Erastus Ethekon, amesema mtu mmoja alifariki dunia katika vurugu zilizozuka wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Ol-Kalou. Emmanuel Too anaripoti kutoka Ol-Kalou.
