"CHAGULAGA" Mila ya Kisukuma Inayokemewa Kupinga Ukatili wa Kijinsia, Dreams Yatumia Siku 16 Mbarali

Mratibu wa Mpango wa Dreams Anusiata Mwamengo amezungumza katika kukamilisha siku 16 za kupinga ukatili kwa wasichana na wanawake, ni katika kikao kilichowahusisha wadau mbalimbali wa kupinga masuala ya ukatili na unyanyasaji. Mila ya CHAGULAGA inayotekelezwa na kabila la Wasukuma wanaoishi wilaya ya Mbatrali Mkoani Mbeya ndiyo imewafanya kuendelea kutoa elimu ili kupunguza na kukomesha kabisa suala la ukatili kwa wasichana hususani kuolewa katika umri mdogo. Majina kwenye Video: 1. Anusiata Mwamengo - Mratibu wa Mpango wa Dreams 2. Blastus Minu - Kaimu Afisa Mtendaji Kata ya Igava 3. Missana Kwangula - Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali 4. Sheikh Ayoub Shupavu - Mdau