Spika Ndugai: Ipo haja ya kusitisha malipo yoyote ya Tundu Lissu

Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema ipo haja ya kusitisha malipo yoyote kwa wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa kuwa Bunge halina taarifa zake rasmi za kuumwa na kwamba amekuwa akifanya ziara nje ya nchi. Spika ametoa kauli hiyo alipokuwa akijibu muongozo wa Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma aliyetaka kujua hatua ya Bunge kwa Lissu ambaye kwa mujibu wa Musukuma, amesema Lissu amekuwa nje ya nchi ‘akizurura’ #AzamTvApp #AzamTvUpdates #TunduLissu