BILLION 30 KWENDA BADILISHA MAISHA MPWAPWA

Waziri wa Maji,Mhe Jumaa H.Aweso amezindua rasmi m radi mkubwa wa Maji wa Badilisha Maisha Mpwapwa wenye thamani ya Shiling Billioni 30 unaofadhiliwa na Shirika la Water For Peole wenye lengo la kuhakikisha huduma za maji safi na salama zinawafikia Wananchi wengi zaid hususani katika vijiji ambavyo havijafikiwa na huduma ya Maji. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Aprili 27,2026 katika Jimbo la Kibakwe wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma ,Mhe Aweso amesema mradi wa Badilisha Maisha Mpwapwa ni sehemu ya utèkelezaji wa Serikali ambapo imelenga kufikisha huduma ya maji katika vijiji 1,557 vilivyosalia hadi kufikia mwaka 2030. Amesema,mradi huo utaenda kunufaisha zaidi ya Wananchi 156,000 katika vijiji 23,pamoja na Shule 11 na vituo vya Afya 10,hata hivyo mradi unahusisha ujenzi wa mifumo 9 ya maji,vituo 255 vya kuchotea maji pamoja na uunganishaji wa maji kwa kaya zenye uhitaji maalum. Utekelezaji wa mradi huo utaengeza upatikanaji wa maji,kupunguza magonjwa yatokanayo na maji yasiyo salama,kuboresha shuhuli za kiuchumi kwa wananchi na kuinua sekta ya elimu amesema Waziri Aweso Halikadhalika,ametoa wito kwa Wananchi,viongozi wa Serikali za Mitaa pamoja na Taasisi husika kuhakikisha wanalinda miundombinu ya maji ili kudumisha uendelevu wa huduma hiyo na kuweza kutumika kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Pia,ametoa shukrani kwa Shirika la Water For Peole Tanzania,kwa kushirikiana na Serikali katika kufanikisha mradi huo,akisistiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali,wadau wa maendeo na jamii ni muhimu katika kufikisha malengo maendeleo endelevu.