Ibada Ya Morning Glory | 10 - 02 - 2025

Karibu katika Ibada ya Masifu ya Asubuhi kutokea hapa kanisa Kuu Azania Front Posta Dar Es Salaam. SOMO: SIKIO LA ROHONI NA UWEZO WA KUMSIKIA MUNGU ANAPOSEMA NA WEWE ~ UFUNUO 1:9 - 11 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu, ▶️MHUBIRI: REV JOASH AILA ....................... KUMBUKUMBU LA TORATI 28: 1 - 6 1 Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; 2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako. 3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani. 4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. 5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga. 6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo. 1 SAMWELI 3:1 -11 1 Basi, mtoto Samweli akamtumikia BWANA mbele ya Eli. Na neno la BWANA lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri. 2 Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona), 3 na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la BWANA, palipokuwa na sanduku la Mungu; 4 basi, wakati huo BWANA akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa. 5 Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena. 6 BWANA akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena. 7 Basi Samweli alikuwa hamjui BWANA bado, na neno la BWANA lilikuwa bado halijafunuliwa kwake. 8 BWANA akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa BWANA ndiye aliyemwita yule mtoto. 9 Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, BWANA; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake. 10 BWANA akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, BWANA; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. 11 BWANA akamwambia Samweli, Angalia, nitatenda tendo katika Israeli, ambalo kila atakayelisikia masikio yake yatamwasha. WAEBRANIA 11:7 Kwa imani Nuhu akiisha kuonywa na Mungu katika habari za mambo yasiyoonekana bado, kwa jinsi alivyomcha Mungu, aliunda safina, apate kuokoa nyumba yake. Na hivyo akauhukumu makosa ulimwengu, akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani. ......................... 👇👇👇 // NAMBA ZA SADAKA // ▶ LIPA KWA [ M-PESA ] - 579 579 4 ▶ NAMBA YA MPESA - 0757 - 391 - 174 JINA: KKKT AZANIA FRONT CATHEDRAL ▶ MAENDELEO BANK A/C NO 0137 9274 6021 JINA: LUTHERAN CHURCH AZANIA FRONT CATHEDRAL TUFUATILIE KWENYE MITANDAO KWA TAHARIFA ZAIDI: Instagram page: / kkkt_azaniafront_cathedral Website: https://www.azaniafront.org/ Facebook: / kkkt-azania-front-cathedral-101434162039079 #azaniafrontcathedral #ibada #lunchhour #morningglory #sundayservice #lutheran