Dizasta Vina - Karibu duniani
Visuals for Tanzanian Hip Hop Artist, Songwriter, and Record Producer Dizasta Vina, Performing a record 'Karibu duniani' Off the Album 'A father Figure' Written by Dizasta Vina Music by Dizasta Vina Vocals by Dizasta Vina Mixed and mastered by J'cob Download/Stream Karibu duniani now Audiomack - https://audiomack.com/dizastavina/son... Mdundo - http://mdundo.com/song/5193524 Spotify - https://open.spotify.com/track/0nK0k3... Youtube Music - • Karibu Duniani DISCLAIMER: Images used in this work were for educational purposes, no harm ever intended Lyrics Yeah Huh Nimekuleta duniani bila idhini Tega sikio kwa makini nikueleze Kabla hujabwaga manyanga chini Nataka uijue hii ngoma ndo’ uicheze Nikutoe utumwani Hata uchague dini yako mwenyewe Mimi baba yako kwahiyo naomba nielewe Hauwezi kupata mwingine , kamwe usiendeshwe na pembe zako Maisha yako yako mikononi mwako mwenyewe Naomba uijue hali yetu Umezaliwa na kuwa hapo ni safari ndefu So, kipindi usiote ndefu usivimbe ufumbue macho Kisha uyatazame ya walimwengu ..tazame ya walimwengu Heshimu hili jina la ukoo Linda kama jinsi unavyoilinda hii roho Palipo uzalendo kuna moyo Na uzalendo unaanza na kuwa loyal Tabia ya upole ni shida kuisanifu Lakini amani na hekima ndo" majibu Hasira picha ya karibu inayokuziba usione mbali Kiasi uone tija kuinasibu Sitakuwepo kukupeleka kwenye toy store Ucheze nazo michezo kwenye korido Uwe mpuuzi ushindwe cheza na books Iwe nuksi kiasi uone revolution is not possible Siahidi kuwa baba mkamilifu Napambana japo mi ganda la udhaifu Amani gharama usijingize kwenye bifu Kosea ujifunze ili usiigize utakatifu kuna dini kama mia mwanangu Sijui ipi ni njia mwanangu Uifate ipi sina jibu Ningemfata mola nimuulize mbingu ingekuwa ikaribu Karibu duniani Karibu duniani ah, Karibu duniani Kua ujue tofauti ya halisi na batili kuhakiki na kubashiri Umasikini na utajiri usafiri Uone tofauti ya usafi na ukafiri Kisha ujiulize kama utaasi au utasawiri Tupa uongo mwanangu chukua tija Funga mdomo mwanangu fungua kichwa Punguza mwendo wengi walijifia kwa haraka Kwa sababu ya kukaidi sheria na mamlaka Ikumbuke hii siku umekua baba Uliyasikia majukumu leo umeyajua sasa Mwanaume ulifichwa msosi tambua Kwamba Hauwezi kuheshimu kazi kama hujajua shamba Kabla hujanishusha mi' hadhi kumbuka Nimekufunza nimekufuta kamasi Nimekuvisha kufuli nimeahirisha shughuli Utanizidi kiburi ila hauwezi ukaivuka tamati mwanangu Hamna urafiki na simba na mwanangu Hata akikufundisha kuwinda mwanangu Kuna siku atawinda kisha windo litamshinda Atakosa nyama na utahitaji kumlinda mwanangu, usiue Mbivu mbichi ngumu rahisi na nyepesi Piga kitabu au uingie kijiji cha mapenzi Mwanangu ufuska utaua hadhi yako Nimekupa vyote ninavyovijua kazi kwako Ukweli kuhusu hivyo vyama vya siasa Chumba kimoja usijedanganywa na vitasa Zote game kama drafti drafti Usishangae kuziona kamati zenye kamati Pesa sabuni zitafute kila sku Ukipata usikate watu mwenye fedha ndo' ana kisu Usisadiki kila tabasamu Kati yao kuna halisi kuna haramu Dadisi upate fahamu Karibu duniani karibu duniani Asili haijali usawa tambua hilo Dunia ngumu kuzaliwa tu ni kuwa hero Hakikisha kisomo hakichezi mbali So chunga ngono chunga mikono serikali Kisha uache kuvamia michakato Kama ambavyo ulikoma ziwa la mamaako Cha ndege kiota cha mtu sumu ukiishi nacho bila macho Mwanangu utazikwa siku si zako, heeh Usiwe mnyang’anyi tafuta fungu lako Ukidhurumiwa ujifunze kutokana na uchungu wako Maana utashushwa na utundu wako Poteza mali lakini usipoteze utu wako Pata shida umjue ndugu thabiti Kumjua ndugu si rahisi Usidanganywe na uchungu wa dhiki Pesa ni nguvu lakini hekima ni nguvu zaidi, ah Ungali na afya jiongezee ujuzi Bahati ya jirani nayo usitembelee uchi Usiegemee kuti, kuwa na nidhamu A'fu fadhiri binadamu ila usitegemee mchuzi Kua uone michongo inapofeli Mchungu muhogo muwa mmoko uliozamisha meli Propaganda na zogo na chokochoko Na utapewa uongo ili ujifunze kuiheshimu kweli We Mwafrika hauko simple una nguvu Ni vile uliibiwa history na mzungu Unachonena kinywani ni tija Kuna mstari mdogo kati ya amani na vita Penda kuwa na lugha nadhifu Maneno thabiti yanaunda uaminifu Acha masihara kaza mwendo ado ado Fanya ndoto kuwa malengo na malengo kuwa mpango Goddamn I'm a father now, Yeah I can't believe that I'm a father how? Nimeacha kushangaa shangaa so Nafanya kazi ukue, so you make your father proud Rafiki adhimu ni kazi Mweshimu kama unavyoheshimu wazazi Mweshimu jirani mbwa na binti yake Binti ni mlezi ukimuharibu jua umeharibu kizazi mwanangu Usijechoka kungojea Kamali ni mbaya usije omba kubobea Wajanja walipotea ogopa pombe na madawa Maana mwili mmoja hauna spare Karibu duniani Karibu duniani Karibu duniani

Dizasta Vina - Utaliimba Jina Langu Ft G Nako

Dizasta Vina - Best Friend

THE UNDERRATED CHAPTER📜 | AFANDE SELE: MULLA OBO ANASTAHILI UFALME | DICAZZI ARUDISHA HIPHOP MTAAN |

Sitaki kua tajiri, nataka kufanikiwa

Episode 77 | Mwanajua by Dizasta Vina (Uchambuzi)

A Confession Of A Mad Father

ZUNGU VINA AONESHA UWEZO MKUBWA WA KUCHANA VINA MEZANI THE THRONE

Dizasta Vina - Wachezaji wa timu

Dizasta Vina - Muscular Feminist

SONGA × NIKKI MBISHI × P MAWENGE - UMIZA NDONGA ( Music Visualizer)

Safari Yangu Ya Biashara, Pesa, Investment & Vision | FULL MASTERCLASS

Dizasta Vina - Shahidi

Hatia V

Dakika 10 Za Maangamizi- Dizasta Vina | Planet Bongo I

DIZASTA VINA aachia diss rasmi kwa RAPCHA ‘The Tribulation’, amshutumu kuandikiwa Mistari

Darassa Ft. Ben Pol - Sikati Tamaa (Official Video)

Dizasta Vina - Hatia IV

Hawatuwezi (feat. Enika)

