MSAFARA WA MAREHEMU WAGEUKA ULINGO WA VITA CHUMANI, KILIFI

Vurugu limeshuhudiwa eneo la Tupendane, Chumani Kilifi mapema leo kufuatia tofauti kuhusu utaratibu wa mazishi kati ya familia ya marehemu Leah Mwaka na ile ya mumewe Shukurani Katana. Marehemu Leah Mwaka aliyefariki Mei 2 2025 wiki moja tu baada ya kufunga ndoa ya kufana na kipenzi chake cha monyoni Shukrani Katana, alitarajiwa kupumzishwa leo nyumbani kwa Mumewe, Uyombo wadi ya Matsangoni. Lakini Tofauti zikazuka badaa ya familia ya marehemu Leah kusisitiza mwili wa marehemu kwanza kufikishwa nyumbani kwao Chumani ili familia kutoa heshima zao za mwisho kabla ya kusafirishwa kwa maziko huko Matsangoni. #COCOFM #mionziyacoco #ladhayapwani