E HABARI JUNE 16 2026\DSE YAIDHINISHA GAWIO LA SH 146.21 KWA KILA HISA BAADA YA KUONGEZA FAIDA

SOKO la Hisa la Dar es Salaam (DSE) limeidhinisha utoaji wa gawio la shilingi 146.21 kwa kila hisa kwa wanahisa wake baada ya kurekodi faida baada ya kodi ya shilingi bilioni 2.348 katika mwaka wa fedha uliopita, hatua inayoakisi kuimarika kwa utendaji wa soko hilo na mchango wake katika kukuza uwekezaji na masoko ya mitaji nchini. Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa DSE, Mwenyekiti wa Bodi, Daniel Ole Sumayan, amesema uamuzi wa kutoa gawio hilo unalenga kuongeza thamani kwa wanahisa na kuhamasisha uwekezaji endelevu, huku ukuaji wa shughuli za soko ukiendelea kuimarisha nafasi ya DSE katika uchumi wa taifa.