BENKI KUU TAWI LA ARUSHA WAADHIMISHA MIAKA 60 YA KUASISIWA KWAKE
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Modest Mkude, ameipongeza Benki kuu ya Tanzania BOT kwa kuadhimisha miaka 60 ya utoaji wa huduma za kifedhaNchini, akiipongeza BoT kwa kusimamia vyema sera za fedha, udhibiti wa mfumuko bei Nchini, kusimamia utulivu wa mfumo wa kifedha pamoja na kuchangia uchumi wa Tanzania kwa kipindi cha miaka 60 ya kuasisiwa kwake. "Mafanikio ya Tanzania katika kudumisha udhibiti wa uchumi kwa miongo hii sita hayawezi kutenganishwa na mchango wa Benki kuu pamoja na ushirikiano wake na serikali, taasisi za kifedha na wadau wengine wa maendeleo." Amesema. Mhe. Mkude amebainisha hayo usiku wa Juni 10, 2026 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mount Meru Jijini Arusha, alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla kwenye hafla ya miaka 60 ya BOT iliyoandaliwa na Benki kuu ya Tanzania tawi la Arusha, akisema maadhimisho hayo yawakumbushe pia kwenda sambamba na mabadiliko ya ulimwengu. "Leo tunashuhudia ukuaji wa teknolojia za kidijitali, mifumo mipya ya malipo, huduma za kifedha kwa njia ya kielektroniki na mabadiliko makubwa katika mazingira ya uchumi wa dunia. Katika mazingira haya Benki kuu inawajibu wa kuendelea kuwa taasisi ya kisasa, bunifu na yenye uwezo wa kukabiliana na changamoto mpya huku ikitumia fursa zinazojitokeza kwa manufaa ya taifa." Amesisisitiza Mhe. Mkude. Mhe. Mkude pia amehimiza benki hiyo kuendelea na juhudi zake za kuongeza ujumuishi wa kifedha ili kutoa fursa ya wananchi wengi zaidi kupata huduma za kifedha, nafuu na zenye kuaminika, akisema ni matarajio yake kuwa Benki kuu ya Tanzania itaendelea kuwa kitovu cha ubora, uwazi na uwajibikaji na weledi katika kutekeleza majukumu yake. Kwa upande wake Meneja wa BOT Tawi la Arusha amewashukuru wafanyakazi, Viongozi na wadau waliofanikisha Benki hiyo kufikia mafanikio na hadhi waliyofikia sasa, akisema maadhimisho hayo ya miaka 60 yatakuwa chachu ya kuongeza ari, ubunifu na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yao kwa manufaa ya Watanzania wote.

Panama – England Highlights | Gruppe L, FIFA WM 2026 | sportstudio

How Toilet Bowls Are Made | Amazing Toilet Bowl Manufacturing Process in Pakistan

RC MAKALLA AIPONGEZA HALMASHAURI YA LONGIDO NA HALMASHAURI ZA ARUSHA KWA KUPATA HATI SAFI🇹🇿

Norwegen – Frankreich Highlights | Gruppe I, FIFA WM 2026 | sportstudio

WAHASIBU NA WAKAGUZI WAPEWA ELIMU YA JUU YA MAJUKUMU YA BODI YA BIMA YA AMANA.

WAZIRI MAKONDA AWAVAA CHADEMA BUNGENI | WANAZUNGUKA KUKINANGA CHAMA CHA MAPINDUZI | SISI WAKUBWA

MWALIMU ASIMULIA ALIVYOKATWA MKONO NA MUMEWE, WATOTO WAKE WAONE VIDOGOLE VILIVYOKATWA, WANAFUNZI

Heche Awatabiria Waliofanya Mauaji Oktoba 29 Kukutana na Yaliyomkumba Mnazi Hitler na Wafuasi Wake

VIONGOZI WA TAASISI ZA UMMA KATAVI WAKUMBUSHWA WAJIBU WA KULINDA MALI ZA SERIKALI.

Afghan most Famous Kabuli Pulao | Pakistani Karahi | Biryani recipe | Roasted chicken | Street food

KIBAHA MUNICIPALITY DISBURSES TSH 991.5 MILLION TO SPECIAL GROUPS, BOOSTING LOCAL ECONOMY

The New Face of Nyerere Road Dar Es Salaam in 2026 | new BRT System and 1000+ trees

WANANCHI WA NGORONGORO WAELIMISHWE KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE- DKT. NGUVILA 🇹🇿

"Africa Is DONE Being Exploited" — African Presidents Speak Out | Africa CEO Forum 2026

DC KALLI AINGILIA KATI KERO ZA MADEREVA WA MALORI LONGIDO

Tazama namna “Viwango Business Forum 2026” lilivyofana

ULINZI, USALAMA NA USAF; VITACHANGIA KUKUA KWA UTALII, NA KUFANIKISHA MIKUTAKUTANO YA KIMATAIFA

MERU DC YATOA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU.

Idi Amin Was A Wise Man | Thabo Mbeki

