NCHIMBI: TANZANIA YALENGA KUWA KITOVU CHA BIASHARA NA VIWANDA AFRIKA, AHIMIZA 'MADE IN TANZANIA'
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imedhamiria kujenga uchumi shindani wa viwanda ili kuifikisha nchi kwenye kipato cha kati cha juu. Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo za Jubilei ya Dhahabu ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) iliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam. Amesema katika kufikia azma hiyo, Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji kwa kiwango kikubwa, utungaji wa sera sahihi, ujenzi wa miundombinu, uimarishaji wa Taasisi na kuwezesha sekta binafsi kufanya biashara kwa ufanisi zaidi. Makamu wa Rais amesema, katika kipindi cha miaka 50 iliyopita, Maonesho ya Sabasaba yamejenga msingi wa ushindani kibiashara, yamechochea ukuaji wa biashara na kujenga uwezo wa wafanyabiashara na wazalishaji, na kuimarisha uhusiano baina ya wazalishaji na walaji. Amesema katika safari ya kuelekea mwaka 2050, maonesho hayo yanapaswa kuwa miongoni mwa maonesho makubwa zaidi ya biashara duniani, yakiiweka Tanzania kama kitovu cha biashara, uwekezaji, ubunifu na viwanda barani Afrika. Halikadhalika, Makamu wa Rais ametoa wito kwa wazalishaji wote nchini kuitumia ipasavyo alama maalum ya bidhaa za Tanzania, yaani Made in Tanzania iliyoanzishwa hivi karibuni ili kujenga hadhi ya bidhaa za Tanzania na kuongeza ushindani wake katika masoko ya Afrika na duniani. Makamu wa Rais amesema ili kutoa mchango stahiki katika utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050, ni vema kufanya mabadiliko makubwa zaidi katika sekta ya viwanda na biashara, ikiwemo uzalishaji wa bidhaa zenye thamani kubwa, na kutumia teknolojia za kisasa katika uzalishaji. Amesema ni muhimu kuongeza ubunifu ili kuanzisha kampuni zitakazozalisha bidhaa zenye ubora na ushindani katika masoko. Aidha, amesema masuala ya utafiti, ubunifu na matumizi ya akili unde, biashara za kidijitali na mifumo ya kisasa ni lazima viwe sehemu ya ukuaji wa uchumi. Vilevile, Makamu wa Rais ametoa rai kwa Taasisi za fedha kujielekeza zaidi kusaidia katika kutoa mitaji kwa sekta ya viwanda, hususan viwanda vidogo vidogo kwa kuweka masharti ya mikopo ya upendeleo kwa viwanda vidogo na

Imihanda yo mu Mujyi wa Kigali yadindiye || Ivugurura mu yubakwa n'abaturage

Biashara zafungwa, usalama waimarishwa Tanzania na Kenya zikiadhimisha 7/7. Katika Dira ya Dunia TV.

MBUNGE MUSUKUMA AKIELEZA MAGUMU ALIYOPITIA KATIKA SIASA NA BIASHARA | M&S PODCAST

PROFESSOR KITILA MKUMBO CALLS FOR A NEW CONSTITUTION | CLAIMS THE CURRENT ONE IS FOR A SINGLE-PAR...

WATCH: Trump says in Zelenskyy meeting that U.S. will allow Patriot missiles to be made overseas

KAULI ya RC CHALAMILA na AFANDE MULIRO KWENYE MAONESHO ya SABASABA...

“TUTAWASHUGHULIKIA WAANDAMANAJI, MWENYE USHAHIDI WA WATEKAJI ANILETEE” - WAZIRI KATAMBI

DUMA BOKO DROPS A BOMBSHELL IN CAPE TOWN! African Leaders Didn't Expect This

HABARI KUBWA JIONI HII KUTOKA TANZANIA...

MAKAMU WA PILI WA RAIS: ZANZIBAR IJIKITE KATIKA KILIMO CHA KISASA NA BIASHARA

WAZIRI KATAMBI KUHUSU TAREHE SABA, ASIMAMIA MSIMAMO WAKE ULE ULE

Air Tanzania Cockpit Boeing 767-300 Freighter to Kinshasa

Africans Must Build Africa | Africa's Richest Man Aliko Dangote’s Bold Message To Other Africans

Asking Africa’s Richest Man How He Made $30 Billion!

How Rwandan Refugees SECRETLY Built a Rebel Movement in Uganda & Kenya | Tharcisse Karugarama

I AM MARWA on Building a Multi Million Estate in the Village, Heartbreak & What It Took to Get Here

UN Secretary-General, Antonio Guterres, opening remarks at the Global Dialogue on AI Governance

DKT. KHALID ATOA UFAFANUZI KUHUSU UWEKAJI TAA BARABARA YA KARIYAKO HADI MAKUNDUCHI

Museveni sits with Dangote and Ruto on a panel to discuss African Infrastructure for development

