JKU yafungua jengo jipya la hospital

Naibu waziri wa Afya Mh Harus Said Sleman amewataka waguzi wa kituo cha Afya cha Jeshi la Kujenga uchumi Jku kutoa lungha nzuri kwa wagonjwa pale yanapotoa huduma ya kwa jamii. Wito huo ameutoa leo wakati alipokuwa akifungua jengo jipya la kutuo cha Afya cha Jku saaten ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra ya kutimiza miaka ,42 ya kuasisiwa jeshi hilo. Mh Harusi ameitaka jamii kuitumia hospital ya Jeshi ya jeshi hilo kwani hospital hjyo ina wataalam wa kutossha na wenye fani tofauti jambo ambalo linapelekea kuondokana na msongamano wa wagonjwa hospital kuu ya mnazi mmoja. Nae mkuu wa jeshi la kujenga uchumi Jku kanali Ali Mtumweni Hamadi ameishukuru Wizara ya Afya kwa juhudi kubwa walioionyesha na kuiomba Serikali kuipatia vifaa vya kisasa ili iweze kutoa huduma bora za uhakika kituoni hapo. Kwa upande wake mganga mkuu wa hospital hiyo luteni kanal machano Isaa Mohd amesema licha ya kuwa na mafanikio lakini pia kuna changamoto zinazo tukabili kituoni hapo ikiwrmo ipungufu wa wataalam wa Afya Vifaa tiba na upatikanaji wa dawa kwa uhakika. Jengo hilo limejengwa kwa nguvu za wana Jku wenye na limegharimu hadi kumalizika kwake ni sh za kitanzania milioni mia moja na hamsini