WANANCHI 2,823 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI BAMBA MWARONGO
Wananchi 2,823 wa vijiji vya Bamba Mwarongo na Mazola Kilifi, Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, wanatarajiwa kunufaika na huduma ya maji safi na salama kufuatia uzinduzi wa mradi wa upanuzi wa huduma ya maji uliofanywa na Mwenge wa Uhuru 2026. Mradi huo umeanzishwa kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji na kusogeza huduma hiyo karibu na wananchi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, za kuboresha huduma za maji na kumtua mama ndoo kichwani. Akiwasilisha taarifa ya mradi mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mkinga, Mhandisi Bakari Kiwitu, alisema mradi huo umehusisha ulazaji wa mabomba kwa umbali wa kilomita 14.214, ujenzi wa tanki la maji lenye uwezo wa kuhifadhi mita za ujazo 75 juu ya mnara wenye urefu wa mita 12 pamoja na ujenzi wa vituo saba vya kuchotea maji. Alisema mradi huo umegharimu shilingi 498,414,502 na unatarajiwa kuboresha maisha ya wananchi wa vijiji hivyo kwa kuwaondolea adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji. Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mkinga, Mhe. Twaha Mwakioja, alisema hali ya upatikanaji wa maji katika jimbo hilo inaendelea kuimarika kutokana na miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali. Alisema kwa sasa kiwango cha upatikanaji wa huduma ya maji katika Jimbo la Mkinga kimefikia asilimia 72.6 na kinatarajiwa kuongezeka hadi asilimia 85 ifikapo Desemba 2026. Mhe. Mwakioja aliongeza kuwa kati ya vijiji 85 vilivyopo jimboni humo, vijiji 77 tayari vinapata huduma ya maji safi na salama, huku juhudi zikiendelea kuhakikisha vijiji vilivyosalia vinafikiwa na huduma hiyo muhimu. Akizungumza baada ya kuzindua mradi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, amepongeza Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika miradi ya maji inayoboresha maisha ya wananchi na kuimarisha huduma za kijamii. Wananchi wa Bamba Mwarongo na Mazola Kilifi wameeleza kufurahishwa na mradi huo wakisema umeondoa changamoto kubwa ya upatikanaji wa maji na utaongeza muda wa kushiriki shughuli za uzalishaji mali na maendeleo ya familia zao.

Makampuni 408 Yaruhusiwa Rasmi Kusafirisha Mazao na Bidhaa za Kilimo Kwenda Nchini China

MWENGE WA UHURU WALIZISHWA NA MRADI WA MAJI LUDEWA KILINDI

WANANCHI WANUFAIKA NA UJENZI WA DARAJA LA USAMBARA LUSHOTO

RC TANGA AUNDA KAMATI KUCHUNGUZA UVUNJWAJI WA NYUMBA KIJIJI CHA MSAKANGOTO, MUHEZA

SERIKALI YATOA MAEKELEZO KWA WANANCHI WA WESTERN—LUHAFWE| HUDUMA ZENYE UTU KUWEZESHWA

JIJI LA TANGA LAWEKA MIKAKATI IMARA KUFIKIA MALENGO 2024-2025.

RC MRINDOKO ASIFU TANGANYIKA DC KUANDAA ENEO LA MAONESHO YA NANENANE, AONYA WAVAMIZI WA ARDHI

Mradi wa Handeni, Korogwe, Muheza na Pangani umefikia asilimia 74 ya utekelezaji wake.

WANAWAKE TANGA WAPONGEZA SAMIA ARDHI KLINIKI KURAHISISHA UPATIKANAJI WA HATI

TANGA YAANDIKA HISTORIA MPYA YA KIBIASHARA

MRADI WA MAABARA WABORESHA HUDUMA ZA AFYA HANDENI MJI

Worst Plane Landing Fails Caught on Camera

See How a 453kg Giant Bluefin Tuna Is Flawlessly Carved in Seconds

MELI YA MAFUTA YA KIMATAIFA YAFIKA ZANZIBAR KUTOKA SAUDIARABIA

15 serbë shanë Shqipërinë, sipërmarrësi nga Lepusha: janë të paguar për provokim

This unusual philosopher will put an end to 10 years of separation

WHEN THE CROCODILE MEETS THE LION DRINKING WATER

YOU Won’t Believe This 😱 Homeless 8 Years of Hair & Beard Transformation

I have never eaten such delicious zucchini! Nobody knows this recipe! Only 2 ingredients!

