Watu sita wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za ufukuaji wa makaburi.

Watu sita wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za ufukuaji wa makaburi na mauaji unaofanyika  wilayani MANYONI Mkoani SINGIDA na mkoa jirani wa TABORA. Watu hao wamekamatwa kufuatia msako mkali uliofanywa na jeshi la polisi wilayani MANYONI na kufanikiwa kuwatia mbaroni watu hao ambao wamekiri kuhusika na tukio moja la mauaji ya mtu mmoja lilitokea mwanzoni mwa mwezi huu wilayani MANYONI.