Waziri Dkt. Stergomena Akabidhiwa Ofisi Rasmi

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb), amekabidhiwa rasmi Ofisi pamoja na shughuli za Wizara. Makabidhiano hayo yamefanyika baina yake na Mheshimiwa Innocent Lugha Bashungwa aliyeteuliwa na Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassana kuwa Waziri wa Ujenzi. Makabidhiano baina yao yamefanyika leo tarehe 04 Septemba, 2023 katika Ukumbi wa Wizara - Mtumba jijini Dodoma, na kushuhudiwa na Menejimenti ya Wizara, tukio ambalo limeenda sambamba utiaji saini Hati ya Makabidhiano. Akiongea na Menejimenti ya Wizara mara tu baada ya kumalizika kwa shughuli ya kukabidhiana ofisi, Mheshimiwa Dkt. Stergomena ameishukuru Menejimenti pamoja na watumishi kwa ujumla wao kwa mapokezi mazuri aliyoyapata alipowasili Wizarani hapo na kuwaomba wampe kila aina ya ushirikiano atakaouhitaji katika kutekeleza majukumu yake kama walivyofanya kwa mtangulizi wake. Aidha, amemshukuru Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Bashungwa kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa kipindi chote tangu alipomkabidhi ofisi tarehe 03 Oktoba, 2022 wakati alipoteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, miezi kumi na moja iliyopita na kumhakikishia kuwa atayaendeleza yale yote aliyoyaacha. Vile vile, Dkt Stergomena amemweleza Mheshimiwa Bashungwa kuwa, kwa anaendelea kuwa Waziri wa Wizara ya Ujenzi, ni matumaini yake kuwa wataendelea kushirikiana naye katika kulisukuma mbele guruduma la maendeleo ya Taifa katika kumsaidia Mheshimiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu katika kuliongoza taifa na kuwaletea maendeleo watu wake. Naye, Waziri wa Ujenzi Mhe. Bashungwa amemshukuru Rais na Amiri Jeshi Mkuu, kwanza, kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuiongoza vyema nchi yetu, pili, kwa kuendelea kumuamini na kumteua kuwa Waziri mpya wa Wizara ya Ujenzi na tatu, mbali na kumteua yeye, ameendelea kumuamini pia Dkt. Stergomena na kumhamisha kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ili aweze kumsaidia katika kuiongoza Wizara ya Ulinzi na JKT. Waziri Bashungwa amemuahaidi Waziri Dkt. Stergomena kumpa ushirikiano wakati wote atapohitajika kufanya hivyo na kumtakia utendaji mwema wa majukumu yake. Aidha, amewahakikishia kuwa Wizara ya Ujenzi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa kuwa Menejimenti na Watumishi wakiwa bado ni Watumishi ataendelea kushirikiana nao kwa karibu zaidi. Kwa namna ya kipekee, Mheshimiwa Bashungwa amewashukuru watumishi wa Wizara, kwa upendo na ushirikiano mkubwa waliompatia wakati wote, uliomwezesha kutekeleza

UAPISHO, Jionee Tukio la Kuapishwa Mkuu wa Majeshi Jacobo Mkunda na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi
▶︎

UAPISHO, Jionee Tukio la Kuapishwa Mkuu wa Majeshi Jacobo Mkunda na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi

Historia ya Hayati Luteni Jenerali Silas Mayunga Vita Vya Kagera.
▶︎

Historia ya Hayati Luteni Jenerali Silas Mayunga Vita Vya Kagera.

WAZIRI WA ULINZI NA JKT DKT. STERGOMENA ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA KAMANDI YA JESHI LA AKIBA MANYONI
▶︎

WAZIRI WA ULINZI NA JKT DKT. STERGOMENA ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA KAMANDI YA JESHI LA AKIBA MANYONI

Haya Ndo Maneno Ya Mke Wa Kikwete Kwa Mumewe Kama Birthday Wishes. | HappyBirthDay JK
▶︎

Haya Ndo Maneno Ya Mke Wa Kikwete Kwa Mumewe Kama Birthday Wishes. | HappyBirthDay JK

HAWA NDIYO WALIMU WALIOMFUNDISHA NAIBU WAZIRI MKUU MHE. DOTO BITEKO
▶︎

HAWA NDIYO WALIMU WALIOMFUNDISHA NAIBU WAZIRI MKUU MHE. DOTO BITEKO

Hotuba ya uzinduzi wa Bunge la 11 dodoma Nov 20,2015
▶︎

Hotuba ya uzinduzi wa Bunge la 11 dodoma Nov 20,2015

WAZIRI MKUU ANAZUNGUMZA NA WANANCHI WA WILAYA YA CHAMWINO MKOANI DODOMA
▶︎

WAZIRI MKUU ANAZUNGUMZA NA WANANCHI WA WILAYA YA CHAMWINO MKOANI DODOMA

KIKWETE ASIMULIA SWALI ALILOULIZWA NA MJUKUU WAKE "KWANINI MAGUFULI KACHUKUA KAZI YAKO?"
▶︎

KIKWETE ASIMULIA SWALI ALILOULIZWA NA MJUKUU WAKE "KWANINI MAGUFULI KACHUKUA KAZI YAKO?"

UCHAMBUZI: SABABU ZA BASHUNGWA KUHAMISHWA WIZARA MARA KWA MARA - "MIAKA 4 WIZARA 5 TOFAUTI"
▶︎

UCHAMBUZI: SABABU ZA BASHUNGWA KUHAMISHWA WIZARA MARA KWA MARA - "MIAKA 4 WIZARA 5 TOFAUTI"

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI JENERALI MABEYO ALIVYOAGA WIZARA YA ULINZI NA JKT ALIMWAGIA SIFA JWTZ
▶︎

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI JENERALI MABEYO ALIVYOAGA WIZARA YA ULINZI NA JKT ALIMWAGIA SIFA JWTZ

WAZIRI WA ULINZI NA JKT ATEMBELEA KAMANDI YA JESHI LA ANGA
▶︎

WAZIRI WA ULINZI NA JKT ATEMBELEA KAMANDI YA JESHI LA ANGA

HILI NDILO BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI
▶︎

HILI NDILO BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI

WAZIRI BASHUNGWA AKIMWAGIA SIFA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI -NDC AONGEA NA MAAFISA NA ASKARI
▶︎

WAZIRI BASHUNGWA AKIMWAGIA SIFA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI -NDC AONGEA NA MAAFISA NA ASKARI

RAIS SAMIA AMUONYA BASHUNGWA - "TUSILEANE, NIPO 'SIRIAZ', UTALIA WEWE"
▶︎

RAIS SAMIA AMUONYA BASHUNGWA - "TUSILEANE, NIPO 'SIRIAZ', UTALIA WEWE"

LEMA Asimulia GWAJIMA ALIVYOMWAMBIA LISSU "Usiende Dodoma, Utapigwa RISASI"
▶︎

LEMA Asimulia GWAJIMA ALIVYOMWAMBIA LISSU "Usiende Dodoma, Utapigwa RISASI"

BREAKING! SAMIA KUMNG'OA NCHIMBI PUNDE | HOJA YA KUTOKUWA NA IMANI NA MAKAMU KUWASILISHWA BUNGENI
▶︎

BREAKING! SAMIA KUMNG'OA NCHIMBI PUNDE | HOJA YA KUTOKUWA NA IMANI NA MAKAMU KUWASILISHWA BUNGENI

WAZIRI MKUU ANAZUNGUMZA NA WANANCHI WA WILAYA YA CHAMWINO, MKOANI DODOMA
▶︎

WAZIRI MKUU ANAZUNGUMZA NA WANANCHI WA WILAYA YA CHAMWINO, MKOANI DODOMA

BASHUNGWA AKIAPISHWA KUWA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA
▶︎

BASHUNGWA AKIAPISHWA KUWA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA

🔴#LIVE: Mapokezi ya Dkt. Stergomena Tax, Wizara ya Ulinzi na JKT
▶︎

🔴#LIVE: Mapokezi ya Dkt. Stergomena Tax, Wizara ya Ulinzi na JKT

MAAFISA UCHUNGUZI WANAFUNZI WA TAKUKURU WAASWA KUPAMBANA NA VITENDO VYA RUSHWA KWA MASLAHI YA TAIFA
▶︎

MAAFISA UCHUNGUZI WANAFUNZI WA TAKUKURU WAASWA KUPAMBANA NA VITENDO VYA RUSHWA KWA MASLAHI YA TAIFA