HATIMAYE KESI YAFIKA MAHAKAMANI WALIOKAMTWA KWA TUHUMA ZA UTAPELI WA NIDA KWA WANANCHI WA LULEMBELA.
WATUHUMIWA WA UTAPELI WA NIDA LULEMBELA WAFIKISHWA MAHAKAMANI KUJIBU MASHITAKA HATIMAYE KESI YAFIKA MAHAKAMANI WALIOKAMTWA KWA TUHUMA ZA UTAPELI WA NIDA KWA WANANCHI WA LULEMBELA. Watuhumiwa wawili waliokuwa wakishikiliwa na Jeshi la Polisi katika Kituo cha Polisi Lulembela, wilayani Mbogwe mkoani Geita kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya udanganyifu, wamefikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayowakabili. Akizungumza mbele ya wananchi, Afisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Wilaya ya Mbogwe, ndugu Erasto Munishi, amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Yona Gazeri (40), mkulima na mkazi wa Katoro wilayani Geita, pamoja na Emmanuel Daniel (35), mkazi wa Kijiji cha Lulembela. Amesema watuhumiwa hao walikamatwa kwa tuhuma za kujifanya watumishi wa Serikali na maafisa wa usajili wa NIDA, wakitumia kivuli cha zoezi la usajili wa vitambulisho vya taifa kwa lengo la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kinyume cha sheria na taratibu, huku akisisitiza kuwa huduma za NIDA hutolewa bila malipo. “Watuhumiwa hawa walikamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya dola, na kwa sasa tayari kesi yao iko mahakamani kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazowakabili,” amesema Munishi. Kwa upande wake, Afisa Mtendaji wa Kata ya Lulembela, ndugu Lazaro Finias Kahabi, akizungumza kwa niaba ya Serikali, amewahimiza wananchi kufuata taratibu sahihi wanapohitaji huduma za Serikali kwa kufika katika ofisi husika ili kupata maelezo sahihi kutoka kwa maafisa wanaohusika, na hivyo kuepuka kudanganywa na matapeli wanaotumia jina la Serikali kuchafua taasisi zake. Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Kata ya Lulembela Nelson Myamchele ameipongeza Serikali kwa hatua madhubuti zilizochukuliwa dhidi ya watuhumiwa hao, akisisitiza kuwa sheria ichukue mkondo wake ili iwe fundisho kwa wengine wenye nia ya kufanya vitendo kama hivyo. Wananchi wa Kata ya Lulembela wamepokea hatua hiyo kwa kuridhishwa, wakieleza kuwa kabla ya kukamatwa kwa watuhumiwa hao, kumekuwepo na malalamiko baadhi yao walikuwa wakitozwa fedha kati ya shilingi 10,000 hadi 20,000 kwa kisingizio cha kupata huduma ya haraka, kabla ya kiwango hicho kupunguzwa hadi shilingi 5,000. Hatua ya kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa hao inaonekana kurejesha imani ya wananchi kwa Serikali na taasisi zake katika kusimamia haki na kulinda maslahi ya umma. #mbogweupdates #mfianchi #amkatanzania

Princess Of Boogie Woogie Delights Everyone

ECU is MESSING WITH HOLGER! 😮💨

The Gallery of Ruto's Lies PART 2: Kenyans furious as Ruto’s promises turn into empty projects

Shùt Up! Former Subin MP Exp0ses Gabby Over His Comment; Captain Smart, Solomon & Hon Kubi React

“You’ll Never Be Like Us.” Until 500KG Happened 🔥

KERO ZA WANANCHI TARAFA YA SUBA ZAPATIWA MAJIBU

WANANCHI LULEMBELA WAISHUKURU SERIKALI KWA KUTATUA CHANGAMOTO YA VITAMBULISHO VYA NIDA LULEMBELA.

HARIANA Today, I am proud to officially launch the #PeaceForDRCNow campaign.

Révision de la Constitution en RDC : Jusqu’où ira le bras de fer entre la CENCO et Félix Tshisekedi?

"DON'T THREATEN ME": HECHE RESPONDS TO MINISTER KATAMBI IN MPANDA, Reveals the Whole Story

KERO LA MAJI SALAITA

Démission, Revirement de Diomaye...: Grosses Révélations de Cheikh Thioro Mbacké

National Assembly: Before the Minister - Guy Marius attacks Diomaye: "He shouldn't have let Macro...

AMAMA MBABAZI ON GEN. MUHOOZI | Erias Lukwago | Muhoozi | Museveni | Besigye

Why Russia is Suddenly Losing in Ukraine

QUANAMINTHE, HAITI 🇭🇹 2026 | Real Streets & Border Life You’ve Never Seen Before#haiti #sosua

BOSOLO NA POLITIK OFFICIAL | JUNE 25 | WITH PROFESSOR BONIFACE KABISA MUSAMBI

MHE MBUNGE KANONI AKIHUTUBIA WANANCHI MADIBIRA

RESTORING THE ORDER 2026 - DAY-6 #dunsinoyekan #worship #intimacy

