NITEMBELEE YESU - Gabriel C. Mkude || St. Cecilia - Babadogo

Watch and listen to the fine tunes of Wanasecilia Babadogo as they perform Gabriel Mkude Sekulu's Nitembelee during mass at Sacred Heart of Jesus Parish - Babadogo || Palm Sunday Year A. ENJOY! SONG: Nitembelee Yesu COMPOSER: Gabriel Mkude Sekulu DIRECTOR: Henry Kings ORGANIST: ‪@odhiswright‬ CAMERA: Bonnie CHOIR: St. Cecilia Choir - Babadogo Ulikuwa na mimi wakati wa shida na wakati wa furaha yangu, Kwa mkono wako ukaniongoza na sasa ninaomba tena, Nitembelee, nitembelee tena, nitembelee mwokozi wangu 1. Ulikuwa pamoja nami, katika mapito yangu, Hukuniacha niangamie, mimi niliye mdogo. Katikati ya safari yangu, nilihisi umeniacha, Uje uje Yesu wangu, nitembelee. 2. Umekuwa mfariji wangu wakati wa magumu, Nikuitapo wakati wowote unaitika. Tazama na adui zangu unawaaibisha, Naomba uje mwokozi Yesu nitembelee. 3. Njoo njoo, Bwana Yesu ninakuhitaji, Niendapo, nipitapo, wewe kinga yangu, Ndiwe faraja ya moyo wangu, mimi nisiyesitahili, Uje Bwana mwokozi wangu nitembelee Bwana. Ninajua unanikumbuka, hujanicha mpweke, Uje Bwana mwokozi wangu, nitembelee. 4. Nawaombea na wale waliokata tamaa, Ili nao wajue ya kuwa upo kati yao. {Waguse Bwana, mwokozi wangu, wajue kuwa wewe upo} Waguse tena, mwokozi wangu watembelee!*2 #youthforchrist #youthministry #wanasecilia