WAKILI WA SERIKALI KUTOKA WIZARA YA KATIBA KUFIKISHWA MAHAKAMANI KISA KUINGILIA MGOGORO WA ARDHI
WAKILI WA SERIKALI KUTOKA WIZARA YA KATIBA KUFIKISHWA MAHAMANI AKIENDELEA KUINGILIA MGOGORO WA ARDHI MBEYA Mvutano kati ya wakili wa kujitegemea Philip Mwakilima na wakili wa serikali kutoka wizara ya katiba na sheria Julius Lukumai unatokana na shauri namba 000014586 la mwaka 2025 kati ya Vumilia Abel Masagati dhidi ya Mage Masagati Mwambugha shauri linalohusu mgogoro wa ardhi katika kijiji cha Hatwelo halmashauri ya wilaya ya Mbeya mkoani Mbeya ambapo Vumilia Abel Masagati alishinda shauri hilo umechukua sura mpya baada ya wakili wa kujitegemea Philip Mwakilima kusisitiza kuwa atamfungulia mashtaka wakili wa serikali kutoka wizara ya katiba na sheria Julius Lukumai iwapo ataendelea kuingilia mgogoro huo. Siku chache zilizopita wakili wa kujitegemea Philip Mwakilima alieleza kuwa atachukua hatua dhidi kile ya alichokiita kikundi cha watu wanaokaa vikao katika ofisi za umma na kutaka kubatilisha maamuzi yaliyotolewa na mahakama.
