HISTORIA YA AICT KWA KIFUPI NA MWANZO WA UONGOZI WA DAYOSISI ILI KUISAMBAZA AICT NCHINI TANZANIA

Mwanzo wa Madhehebu ya AIC Kenya na Tanzania unaanzia kwenye karne ya 18/19 kupitia wamissionari wa AIM (Africa Inland Mission) kisha 1909 AIM walipoingia Tanganyika iliyokuwa ikijulikana kama Germany East Africa nyakati zile. Mnamo mwaka 1909 wamissionari wengine madhehebu ya CMS (Christian Mission Society) walikuwa tayari walishapiga kambi Tanganyika eneo la Nassa, Magu Mwanza. Safari ya AIM kuja Tanganyika waliingilia hapa Nassa baada ya CMS kuamua kurudi kwao Marekani na kuwaachia AIM kuendeleza utume mahali hapo ambapo baadaye AIM walikabidhi majukumu haya kwa wazawa wa hizi nchi mbili za Kenya na Tanganyika, na kuwa AIC. Kenya wakawa AICK na Tanganyika baadaye Tanzania wao wakawa AICT. Tangu hapo 1909 utume wa madhehebu haya kwa upande wa Tanganyika ukaendelea kusambaa kidogo kidogo ukieneza Injili pamoja na huduma za kijamii kama Vyuo vya kufundisha watumishi wa Neno la Mungu, Shule za elimu ya kawaida pamoja na Hospitali karibu kila sehemu walipoweka kambi. Kwa sasa hivi AICT baada ya kuanzisha Uongozi wa Dayosisi, imesambaa Mikoa mingi nchini Tanzania na upande wa Magharibi AIC imepenya hadi nchi jirani ya Rwanda. Bila shaka sasa huko panakwenda kuwa na AICR. Mungu ibariki kazi hii ya kuisambaza Injili ya mwanao Yesu Kristo, Jina Kuu lipitalo majina yote mbinguni na duniani isambae duniani kote.