Nyimbo za Wokovu 51 : Naona Amani Golgotha | Tabernacle de Likasi

Nyimbo za Wokovu 51 : Naona Amani Golgotha | Tabernacle de Likasi 1. Naona amani Golgotha Alipojitoa Mwokozi, [ Na huko nina kimbilio Kwa Yesu aliyenipenda. ] BIS 2. Sitaki ’tamani fahari Na dhambi katika dunia, [ Sababu wokovu ninao Katika ’jeraha ya Yesu. ] BIS 3. Aliziondoa kabisa mizigo na kamba ya dhambi. [ Na niliokoka halisi Kwa Neno la Mungu wa ’hai. ] BIS 4. Maneno ya Mungu ni kwetu Chakula na dawa ya roho, [ Na nguvu ya kusaidia Mkristo katika safari. ] BIS 5. Ni sasa hekalu la Roho, Anayemiliki moyoni; [ Na Yesu ananiongoza Kwa njia ya ahadi zake. ] BIS 6. Uliye dhambini ufike Kwa Yesu Mwokozi wa wote ! [ Anakunyoshea mikono Ya pendo kukusaidia. ] BIS Nyimbo za Wokovu 51 : Naona Amani Golgotha | Tabernacle de Likasi #Maranatha