ALIWAONA TABU LEY, FRANCO NI WATESI WAKE

Hii ndiyo Sauti ya gharama katika makala hii ambapo tunachambua wimbo wa Non maarufu kama Non Libala ambao ndiyo kiini au msingi wa Madilu System kuibuka na kujulikana kwenye ulimwengu wa muziki wa Rhumba duniani kote. Wimbo wa Ya Jean maudhui yake yalianzia kwenye wimbo wa Non Libala ambao ulikuwa ni mwanzo wa kung'aa kwa nyota ya Mwanamuziki huyu Madilu System Wimbo wa "Ya Jean" wa Madilu System unamwelezea mwanamke anayelalamika na kusikitika baada ya kuachwa ghafla na mumewe (mwenye jina la Jean (jhzaa au jzhoon) kwa sababu ya wivu wa ndoto tu. Huu ni wimbo wa hisia kali za mapenzi, majonzi, na kilio cha kuomba msamaha. Kwanini Madilu anaomba msamaha? Anamwomba msamaha nani? na Kwasababu gani aombe msamaha katika wimbo huu wenye mafumbo ya kisa cha kweli cha maisha ya Madilu Sytem?